HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 05, 2020

RC TABORA AWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA KILIMO NA UFUGAJI

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akifungua jana kongamano la siku mbili la vijana katika fursa za kilimo , mifugo  na uvuvi ambao wameoka  Tabora, Kigoma na Singida.



NA TIGANYA VINCENT

VIJANA wametakiwa kutumia fursa zinazotokana shughuli za kilimo na ufugaji kujiari wenyewe badala ya kusubiri ajira za Serikali ili wawaze kujiongezea kipato kwa ajili ya maendeleo yao wenyewe na Taifa kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati akifungua kongamano la vijana katika fursa za kilimo , mifugo  na uvuvi kwa washiriki toka Tabora, Kigoma na Singida.

Alisema Serikali kupitia Wizara ya Nishati, imejitahidi kufikisha umeme vijijini ambako ndiko mazao yanapatikana ili kuweza kuyaongezea thamani kwa kuyasindika.

Mwanri alisema hiyo ni fursa nzuri kwa vijana ya kutumia umeme ilikufanya kazi za kuzalisha na kuchakata mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi hivyo kuongeza thamani na uhakika wa soko na bei nzuri.

Alisema uzalishaji wa mbegu bora za mazao nchini una uhitaji mkubwa na takwmi zinaonyesha kuwa mahitaji ya mbegu ni tani 187,000 kwa mwaka wakati uzalishaji wa ndani ni tani 71,000.

Mwanri aliongeza kuwa eneo hilo lina fursa kubwa kwa vijana kuzalisha mbegu kwani zinzhitajika kwa wingi.
Alisema eneo jingine ambalo ni fursa kwa vijana ni kilimo cha mazao ya mafuta ambapo mahitaji ya mafuta ya kula ni lita 650,000 kwa mwaka wakati uwezo wa nchi ni kuzalisha lita chini ya 250,000.

Mwanri alisema hali hiyo inatoa fursa kubwa kwa vijana kuzalisha mazao ya alizeti na michikichi.

Kwa upande wa Mratibu wa Mkakati wa Taifa wa Vijana kushiriki katika Kilimo Revelian Ngaiza alisema lengo kongamano hilo ni kutoa elimu kwa vijana nchini ili waweze kushiriki katika uzalishaji mali kupitia kilimo na ufugaji ili waweze kuinua kipato cha na Taifa kwa ujumla.

Alisema kauli mbiu yetu ni “vijana,kilimo ni ajira” imelenga kuwasaidia vijana kutambua na kufanya kilimo kuwa nguzo ya upatikanaji ajira nyingi zaidi.

No comments:

Post a Comment

Pages