HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 04, 2020

Wateja 1,900 wa Tigo wanufaika Chemsha Bongo

Mtaalam wa Huduma za Kidijitali  kutoka Tigo, Ikunda Ngowi,akimkabidhi mfano wa hundi ya 13m/- mshindi wa promosheni ya Tigo Chemsha Bongo 2020 Miller Said Kungwi, mkaazi wa Mbagala, Dar es Salaam.


Na Mwandishi Wetu
 
WATEJA 1,904 wa Kampuni ya Tigo Tanzania wamejinyakulia shilingi milioni 197.5 kupitia promosheni ya Chemsha Bongo.
Hayo yalisemwa na Mtaalam wa Huduma za Kidijitali wa Tigo, Ikunda Ngowi, wakati akimkabidhi mfano wa hundi mshindi wa jumla ya promosheni hiyo Miller Kungwi kutoka Mbagala jijini Dar es Salaam, aliyeibuka mshindi wa jumla na kupata shilingi milioni 13.
Alisema promosheni hiyo ilianza Oktoba 2018 ambapo Watanzania 1,904 wameshiriki na Kungwi ameibuka mshindi wa jumla hivyo kuwaomba Watanzania kuendelea kushiriki katika awamu ya sita ya promosheni hiyo.
Ngowi alimpongeza mshindi huyo kwa kutumia fursa hiyo na kuwashukuru wateja wote wa Tigo ambao walishiriki na baadhi yao kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo zawadi za fedha taslimu ambazo zinatolewa na kampuni hiyo.
“Tunayo furaha kubwa kumkabidhi mshindi wetu fedha zake. Tunawashukuru wateja wetu nchi nzima walioshiriki kwenye promosheni hii ya miezi mitatu ambayo sasa imemalizika”. alisema Ikunda.

Mtaalam huyo alisema pamoja na fedha pia kupitia promosheni hiyo wametoa simu 30 na gari moja aina ya Renault Kwid lenye thamani ya shilingi milioni 23.
Alisema Tigo imeamua kurejesha fadhila kwa wateja wake na kuahidi kuwa wataendelea kuboresha huduma zao ili wateja wao waweze kufurahi.
“Mwisho wa promosheni hii ni mwanzo wa nyingine hivyo tunawaomba wateja wetu kuendelea kucheza ili waweze kujinyakulia zawadi,” alisema.
Kwa upande wake Kungwi alishukuru kuibuka mshindi na kuahidi kuzitumia katika kufanikisha maendeleo ya familia yake.
Kungwi alisema “Wakati napigiwa simu, nilikuwa nyumbani najipanga kutoka kwenda katika mihangaiko yangu ya kibiashara, nilipopata ile taarifa kwamba nimeibuka mshindi nilifurahi sana, kwani sikutegemea kabisa kuwa ningeibuka mshindi katika promosheni hii.
Habari hizi naziona kama ndoto kwangu, nashukuru Tigo kwa kunipa zawadi hii kwani itanisaidia kujiajiri na kuisaidia familia yangu “alisema.

No comments:

Post a Comment

Pages