HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 25, 2020

NACOPHA YATOA VIFAA VYA KUJIKINGA NA CORONA MKOANI TABORA

NA TIGANYA VINCENT

Baraza la Taifa la watu wanaoishi na VVU (NACOPHA)  limetoa  vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 26 kwa Mkoa wa Tabora kwa ajili ya watu wanaosihi na virusi vinavyosabisha Ukimwi kujikinga na kudhibiti kuenea kwa Virusi vya Corona.

Hatua hiyo inalenga kuwawezesha jamii ya watu wanaoishi na VVU na jamii inayokuwa karibu nao kuweza kuvitumia katika kuchukua hatua za kujikinga na kupata maambukizi ya ugonjwa wa Covid -19.

Vifaa hivyo vimekabidhiwa jana mjini Tabora na Mtendaji Mkuu wa NACOPHA Deogratis Rutatwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri kwa niaba ya Halmashauri zote.
Alisema wametoa sabuni za kunawiana mikoni, vitakasa mikono, vidonge vya kuweka katika maji ya kunawiana . Detto na barakoa.

Rutatwa alisema wameamua kutoa msaada huo ambao wamesaidia na Shirika la Misaada la Watu wa Marekani(USAID)  chini ya kauli mbinu hebu tuyajenge tufiku 95-95-95 ili kuungana na jitihada za Serikali za kukabiliana na janga la Corona kwa watu wanaoishi na VVU.

Alisema pamoja na Mkoa wa Tabora pia wametoa vifaa vya aina hiyo Kigoma, Shinyanga, Geita, Kagera, Mwanza na Mara ili viweza kuwasaidia watu wanaoishi na VVU kujingana na Corona.

Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya Halmashauri nane za Mkoa wa Tabora, Mkuu wa Mkoa huo Mwanri aliishukuru NACOPHA kwa kujali na kuona umuhimu wa kusaidia kundi hilo katika kukabiliana na janga la Corona.

Alitoa wito kwa Mashirika mengine kusaidia vifaa kwa watu wenye mahitaji maalumu kama vile walemavu ili waweze kujinga na Corona.

Mwanri alisema jamii ya watu wenye ulemavu wakati mwingine inahitaji msaada wa mtu wa pili katika kufanya shughuli mbalimbali na hivyo wasipokuwa na vifaa kama vile barakoo, vitakasa mikono wanaweza kupata maambukizi ya Corona.

Aliwaonya watu watakaopewa vifaa hivyo kuvitumia kwa makusudi yaliyokusudiwa na sio kutumia nje ya malengo.

No comments:

Post a Comment

Pages