HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 29, 2020

Kampeni ya Elimisha Kibaha na Benki ya NMB yakabidhi msaada wa mabati 160

 Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Assumphta Mshama (kushoto), akizungumza jambo na  Meneja wa Benki ya NMB kanda ya mashariki, Baraka Ladislaus baada ya kumalizika kwa  utekelezaji wa Kampeni ya Elimisha Kibaha na Benki ya NMB kukabidhi msaada wa mabati 160 katika hafla iliyofanyika shule ya sekondari ya Zogowale mkoani Pwani.     
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Josephat Kandege (katikati), akinong'ona jambo na Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Mashariki, Baraka Ladislaus (kushoto), baada ya benki hiyo kutoa msaada wa jumla ya mabati 160 kwa shule za sekondari Magindu iliyopata mabati 106 na shule ya sekondari Msagani mabati 54 yote yakiwa na thamani ya sh5milioni katika hafla iliyofanyika shule ya sekondari ya Zogowale halmashauri ya wilaya ya Kibaha mkoani Pwani, kulia ni mkuu wa wilaya ya Kibaha, Assumphta Mshama.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Josephat Kandege (kulia), na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Assumphta Mshama (kushoto), wakisikiliza jambo kutoka kwa Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Pwani CCM, Hawa Mchafu katika hafla ya benki ya NMB kukabidhi msaada wa mabati na utekelezaji wa kampeni ya Elimisha Kibaha katika shule ya sekondari ya Zogowale. 
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Josephat Kandege (Mwenye miwani), Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Mashariki, Baraka Ladislaus (wa pili kushoto) na  Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Assumphta Mshama (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa benki hiyo idara ya elimu mkoa wa Pwani baada ya benki ya NMB kutoa msaada wa jumla ya mabati 160 kwa ajili ya shule za sekondari Magindu iliyopata mabati 106 na shule ya sekondari Msagani mabati 54 yote yakiwa na thamani ya sh5milioni wakati wa hafla ya utekelezaji wa kampeni ya Elimisha Kibaha kukabidhi vyumba vya madarasa 32 iliyofanyika shule ya sekondari ya Zogowale mkoani Pwani,
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Josephat Kandege (katikati), akimkabidhi moja ya vikombe 12 Meneja wa benki ya NMB kanda ya mashariki, Baraka Ladislaus kulia baada ya kununua katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa vyenye thamani ya sh240,000 wakati wa hafla ya utekelezaji wa kampeni ya Elimisha Kibaha kukabidhi vyumba vya madarasa 32 iliyofanyika shule ya sekondari ya Zogowale halmashauri ya wilaya ya Kibaha mkoani Pwani, kushoto ni mkuu wa wilaya ya Kibaha, Assumphta Mshama. 

No comments:

Post a Comment

Pages