HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 15, 2021

Hawa ndio wanafunzi 10 bora kitaifa waliofanya vizuri

BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha nne na kutoa orodha ya wanafunzi 10 bora waliofanya vizuri katika mtihani huo.

Akitangaza wanafunzi hao na shule zao za sekondari kwenye mabano leo Januari 15,2021 jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa baraza hilo Dk. Charles Msonde amewataja kuwa ni Paul Luzinga (M) (Pandahili Mbeya), Justina Gerald (F) (Canossa-Dar es Salaam), Timothy Segu (Mzumbe-Morogoro), Isaya Rukamya (M) (Feza Boys- Dar es Salaam).

Wengine ni Ashrafu Ally (M) (Ilboru- Arusha), Samson Mwakabage (M) (Jude-Arusha), Derick Mushi (M) ( Ilboru-Arusha), Layla Atokwete (F)(Canossa- Dar es Salaam), Innocent Joseph (M) (Mzumbe-Morogoro) pamoja na Lunargrace Celestine (F) (Canossa-Dar es Salaam).

Hata hivyo katika matokeo hayo, Shule ya Sekondari Cannosa ndiyo iliyong’ara zaidi kwa kuingiza wanafunzi watatu kwenye orodha ya wanafunzi 10 bora kitaifa.

No comments:

Post a Comment

Pages