HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 21, 2021

Tandale kukuza vipaji vya vijana sekta ya michezo

Na Asha Mwakyonde

DIWANI wa Kata ya Tandale iliyopo Wilaya  ya Kinondoni Chifu Abdallah  Saidi wanatarajiwa kuandaa mashindano yenye lengo la kukuza vipaji vya vijana wa kata hiyo.

Akizungumza jijini Dar es Salaama leo Januari 21, 2021 Chifu  Saidi amesema michezo ni ajira kwa vijana wenye vipaji na wanaojituma kwa kile wanacho kifanya.

Diwani huyo amefafanua kuwa mashindano hayo yatahusisha mpira, Pet, rede na mingine ikiwa ni pamoja na ngumi.

" Niliahidi kutengeneza nyumba ya kukuza vipaji vya vijana wa Tandale ( House of Talent), ili vijana hao waweze kupata ujuzi zaidi," amesema Chifu Saidi.

Amesema mbali na kujitenenezea ajira vijana hao kupitia michezo pia wataweka afya zao katika hali nzuri kutokana na michezo hiyo.

Diwani huyo ameongeza kuwa vijana wapo vijana ambao wamejituma kwa kucheza kwa bidii katika mchezo anaoupenda na kufanikiwa katika maisha yao na kuzisaidia familia zao kiuchumi.

Chifu Saidi ametolea mfano kwa mchezaji Mbana Samatta ambaye amepata mafanikio makibwa ya kucheza nje ya nchi na kuitambulisha Tanzania vema.

Amewataka vijana wa Kata ya Tandale kujitokeza kwa wingi mashindano hayo yatakapoanza ili waonyeshe vipaji vyao na baadae waweze kusaidiwa.

No comments:

Post a Comment

Pages