HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 06, 2021

SIMBA JAMII YAUNDA KAMATI NDOGO NNE


Katibu Mkuu wa Taasisi ya Simba Jamii Tanzania Enterprises (SJTE), Hassan Mohammed (EBS).

 

NA SULEIMAN MSUYA


KAMATI ya Utendaji ya Taasisi ya Simba Jamii Tanzania Enterprises (SJTE), imeunda kamati ndogo nne ambazo zitashirikiana na kamati kuu kufanikisha mipango ya taasisi hiyo kufikiwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa SJTE, Hassan Mohammed (EBS), amesema kamati hizo ndogo zimeundwa baada ya wajumbe wa kamati hiyo kukutana kwa mara ya kwanza siku chache baada ya kuchaguliwa.

"Kamati Tendaji ya SJTE ilifanya kikao cha kwanza chini ya Mwenyekiti Patrick Mwanakatwe na kujadili mambo mbalimbali ikiwemo kuunda kamati, kuteua mweka hazina na uchaguzi wa wajumbe wa kamati ya utendaji," amesema.
 
Katibu mkuu huyo amesema pamoja na Mwenyekiti pia kikao hicho alikuwepo Makamu Mwenyekiti James Tindi, Naibu Katibu Asha Kigundula, Mweka Hazina Zaitun Dagila, Wajumbe wa Kamati ya Utendaji Nunu Rashid, Mussa Mongi na Laurencia Sahani.

Katibu mkuu amezitaja kamati zilizoundwa na Kamati ya Utendaji ni Kamati ya Nidhamu na Maadili itakayoongozwa na Mwenyekiti Hassan Mbilili, wajumbe Mhandisi Said Khalfan, 
Jasmin Badar na Faraj Kimonge.

"Kamati ya Habari, Matukio na Safari ikuwa chini ya Mwenyekiti  Seperatus Kisimba, Katibu Seleman Msuya, wajumbe Asha Kigindula Laurencia Sahani, Cecy Mushi, Adrian Galid, Jacob Mandeje, Leonard Ngomai, Mussa Mongi Chacha Sadalla na Alice Mgaya," amesema.

Aidha Katibu Mkuu ametaja kamati nyingine ni ya Fedha, Uchumi na Mipango chini ya Mwenyekiti Mashaka Kirazi, Katibu Zaituni Dagilla, wajumbe Nunu Rashid, Masoud Ameir, Danny Poul, Dullah Dumea na Dk. Fanuel.

Amesema pia wameunda Baraza la Wadhamini ambalo litaongozwa na Mwenyekiti Mhandisi Said Khalfan, Katibu 
Rahim Varisanga, wajumbe Faraj Kimonge Hassan Mbilili na Nassor Ossama.

Amesema matarajio yao ni kuona kamati hizo ndogo zitashirikiana na Kamati ya Utendaji kusukuma gurudumu la maendeleo.

Mohammed amesema kikao kilitoa maazimio kuwa nafasi mbili za wajumbe wa kamati ya utendaji zijazwe kwenye mkutano unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni. 

"Wajumbe walikubaliana nafasi hizo ziachwe wazi mpaka utakapofanyika mkutano mkuu ujao ili zijazwe kwa wagombea kupigiwa kura na wanachama wenyewe.

Hivyo nafasi hizo ziko wazi na zitatangaziwa utaratibu wa kuzijaza wakati wa mkutano ujao," amesisitiza.

Amesema kuhusu nafasi ya mweka hazina wajumbe wa kamato tendaji kwa kauli moja walikubaliana kuwa  Zaituni Dagilla aendelee kuwa Mweka Hazina wa Simba Jamii mpaka utakapofanyika mkutano  ujao na kusomwa mapato na matumizi ndio nafasi hiyo inaweza kufanyiwa mabadiliko ama la.

No comments:

Post a Comment

Pages