HABARI MSETO (HEADER)


 


Breaking

January 16, 2022

King: kunahitajika Spika mwenye ueledi mzuri


Prof. Norman King.

  

Na Asha Mwakyonde, Dodoma

RAIS wa Taasisi ya Wataalamu wa Utazamaji wa Uchaguzi Afrika(ANEOPI), Prof. Norman King ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Hai,  Moshi amechukua fomu jana ya kuomba kuteuliwa  na chama cha Mapindizi (CCM),nafasi ya Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akizungumza mara baada ya kurudisha fomu hiyo King alisema  lengo la kuchukua fomu hiyo ni kwa sababu ya changamoto ikiwa ni pamoja na muundo wa katiba kubadilika

King ambaye pia  aliwahi kuwa mkuu wa Wilaya za Mbeya na Songea alisema kutokana na mabadiliko  hayo kunahitajika Spika mwenye ueledi mzuri wa kukielewa chama cha CCM vizuri.

"Kwa sasa ni muhimu mabadiliko yakawepo ni lazima Spika awe ni mtu mwenye ufahamu wa kutosha kuweza kukidhi hoja  za wabunge," alisema King.

Aliongeza kuwa kuna watu mashuhuri waliochukua fomu na  kwenye CCM watu hao wapo wengi  yoyote anaweza kuwa Spika  kwa kadri chama kinavyotaka.

No comments:

Post a Comment

Pages