HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 28, 2022

Tanzania kushindana na nchi nyingine ulimwenguni mifumo ya mtandao Mahakama ifikapo 2025


 Jaji Mkuu wa Tanzania,Profesa Ibrahimu Juma akisaini kitabu cha wageni katika moja ya mabando ya maonesho ya wiki ya Mahakama.

 

Na Asha Mwakyonde, Dodoma


JAJI Mkuu wa Tanzania,Profesa Ibrahimu Juma amesema kuwa itakapofika Disemba 31,2025 wawe ni nchi inayoshindana na nchi yoyote ulimwenguni katika masuala ya mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(TEHAMA), ya Mahakama kwa lengo la kuwasaidia wananchi utoaji wa Huduma.

Prof Juma ameyasema hayo  leo Jijini Dodoma mara baada ya kutembelea mabanda mbalimbali yanayoshiriki maonesho ya wiki ya Sheria ambayo Kitaifa yanafanyika kwenye Viwanja vya Nyerere Skwea Jijini hapo  yenye kauli mbiu " Zama za Mapindizi ya nne ya Viwanda. Safari ya maboresho kuelelea Mahakama Mtandao, " amesema kuna haja ya kuboreshwa  kwa mifumo mitandao.

 Pia amesem mifumo ya Mahakama mtandao itawasaidia  wananchi  utoaji huduma na kukuza uchumi kwani  mifumo mingi ya Mahakama kwa Sasa imekuwa na changamoto ya kutosoma na  hivyo kutoleta manufaa kwa wananchi hao.

"Ushindani wa teknolojia tumebakisha miaka minne ya robo ya kwanza itakuwa ni jukumu la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kutayarisha dira ijayo ya miaka 25 ijayo," amesema Jaji Mkuu.


Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa maonyesho hayo akiwemo Afisa Uchunguzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupamabana na Rushwa (TAKUKURU),Grabriella  Gabriel,Mwanasheria wa Chama cha Wanasheria wanawake (TAWLA),Lilian Mollel na Kaimu Katibu wa Tume ya marekebisho ya Sheria Nchini,Zainabu Chanzi wamesema  huduma wanazozitoa katika wiki ya Sheria ni pamoja na msaada wa kisheria
 

No comments:

Post a Comment

Pages