HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 26, 2023

Dirisha la udahili lafunguliwa NACTVET

 Na Mwandishi Wetu


BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limefungua dirisha la udahili wa mkupuo wa mwezi Machi kwa mwaka wa masomo wa 2023/24 kuanzia Januari 16 mwaka huu.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mtendaji wa Baraza hilo imesema kwamba vyuo vyote vinaruhusiwa kudahili wanafunzi katika mkupuo huu, isipokuwa vyuo vinavyotoa mafunzo ya Afya na Sayansi Shirikishi kwa Tanzania Bara.         

Taarifa hiyo imesema vyuo vya Afya na Sayansi shirikishi vilivyopo Tanzania Visiwani vyenye uwezo wa kudahili katika mkupuo huo vinaruhusiwa ikiwa vitakidhi vigezo.

Katika taarifa yake hiyo, NACTVET limevielekeza vyuo vinavyohitaji kudahili wanafunzi kwa mkupuo huu kutuma maombi yao kabla ya Januari 27, 2023 kwa kujaza fomu inayoonesha uwezo wa chuo kuendesha mafunzo na kuiwasilisha katika ofisi za Kanda za Baraza ambapo chuo husika kipo.

“Uwezo huo ni pamoja na kuwa na miundombinu na walimu wa kutosha kutoa mafunzo katika mikupuo miwili kwa mwaka (Machi na Septemba)” imesema sehemu ya taarifa hiyo. 

Baraza hilo limesema kwamba fomu ya maombi inapatikana katika tovuti ya Baraza hilo www.nacte.go.tz kwa kubofya fomu ya maombi ya udahili March Intake 2023/24.              


No comments:

Post a Comment

Pages