HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 24, 2023

IBENGE AFUATA 'UBANI' WA KLABU BINGWA TANZANIA

Kocha wa Al Hilal ya Sudan, Frolent Ibenge, ameamua kuweka kambi nchini Tanzania ambapo watacheza mechi 3 za kirafiki wakijiandaa kwa hatua ya makundi ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika. Mechi hizo watacheza dhidi ya Namungo FC, Azam FC na Simba SC.



Ibenge na vijana wake watakuwa Tanzania kuanzia Januari 25 mpaka Februari 6 ambapo watahitimisha kambi yao hiyo. Al Hilal waliiondosha Yanga katika hatua ya mtoano CAFCL na kufanikiwa kutua hatua ya makundi.


No comments:

Post a Comment

Pages