HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 04, 2024

MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWAFUNDA WADAU WA HABARI DODOMA

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MSEMAJI Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Mobhare Matinyi amesema Serikali itaendelea  kuheshimu na kuimarisha uhuru wa vyombo  vya  habari  nchini  ikiwa ni pamoja na kusisitiza  uwahibikaji utakaowezesha  chaguzi zetu kuwa wazi,jumuishi na zenye  kuheshimika.


" Kwa pamoja tunaweza  kujenga  demokrasia  imara  zaidi ambapo vyombo vya habari  vinakua kichocheo  cha mabadiliko chanya  na maendeleo  ya kijamii" amesema Matinyi. 

Amesema hayo  leo  Aprili 30 Jijini Dodoma  katika mkutano  wa wadau wa habari  kuhusu wajibu  wa vyombo  vya habari  katika  kuhakikisha  kunakuwa na uchaguzi  unao aminika. 



  "Tunaishi katika nyakati  ambazo habari  zinapatikana  na kusambaa kwa urahisi na kwa kasi ya juu sana na hivyo  kukazimu  umakini na usahihi  wa kiwango cha juu hivyohivyo  usambazaji  wa habari  za uongo, upotoshaji na habari zinazosababisha uhasama unaoweza kudhoofisha taswira ya uchaguzi zetu  na kuharibu  imani  ya umma kwa mantiki hii  ni jukumu la kila mdau pamoja vyombo vya habari  kudumisha  viwango vya juu vya weledi kufuatia miongozo ya maadili na kukuza uandishi  wa habari unaowajibika amesema Matinyi.

"Nalipongeza Baraza la Habari Tanzania (MCT) kwa jitihada  zake  katika  kuendeleza  weledi, maadilina uwajibikaji  katika tasnia ya habari  kwani majukumu ya MCT ni kuhakikisha  tunakua na uandishi wa habari  wenye  viwango bora.

Aidha tunahamasisha  uhuru  wa vyombo  vya habari  na wanatetea  haki za waandishi  wa habari ambayo ni majukumu  muhimu katika demokrasia inayostawi ,hivyo wanapaswa kupongezwa"
amesema Matinyi.

Amesema kuwa vyombo vya haba vina wajibu  mkubwa  na  muhimu  katika jamii yoyote yenye demokrasia  kwa sababu mijadala mbalimbali  kwenye umma.


Tunapokaribia  katika  mchakato  wa uchaguzi  jukuku la vyombo vya habari  linakua ni muhimu zaidi  kwa kupitia majukwaa  yenu  ndipo wananchi  wanapopata  habari  habari ikowa ni pamoja na kuelimishwa jinsi ya kusiriki katika  chaguzi  na hivyo kupata  na kutumia  fursa  ya kufanya maamuzi yenye manufaa kwao.
 

No comments:

Post a Comment

Pages