MSANII
wa muziki wa kizazi kipya nchini, Sunday Mangu ‘Linex’ amesema ameghairi
kugombea ubunge mwaka 2020 kama alivyokuwa amepanga kutokana na kuona kwamba
mashabiki wake bado wanamhitaji katika sanaa.
Linex
alishawahi kutamba na ngoma zake kama Mahakama ya Mapenzi, Aifola, Unataka Ndoa
au Harusi na nyinginezo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika tasnia
hiyo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Linex alisema, awali baada ya
kutangaza hivyo alipata maswali mengi sana kutoka kwa mashabiki wake, hivyo
ameamua kuendelea na muziki kwanza.
“Ni
vizuri tukiwa na ndoto za baadae katika maisha yetu, ndoto ya kugombea ubunge
ipo lakini sio 2020 kwasasa naona niendelee na muziki kwasababu nimegundua
kwamba wadau bado wananitaka,” alisema Linex.
Linex
aliwataka wadau wa kazi zake waendelee kumapa sapoti katika muziki wake na
kwamba yupo katika mikakati ya kusambaza ngoma yake mpya ambayo bado hajaipatia
jina na kwamba katika wimbo huo kuna sehemu itasikika sauti ya Mbunge wa Kigoma, Zitto Kabwe.
No comments:
Post a Comment