NA
ELIZABETH JOHN
Chidi Benzi |
MSANII
wa muziki wa kizazi kipya nchini, Rashid
Makwilo ‘Chidi Benzi’ amemshauri nyota wa muziki
huo, Diamond Platinumz asitumie madawa ya kulevya, sigara wala pombe ili
kuendelea kung’ara katika tasnia hiyo.
Diamond Platinumz |
Akihojiwa
katika kipindi cha XXL kinachorushwa na Clouds, Chidi Benzi alisema, ameamua
kumshauri kama mdogo wake na pia anapenda kazi zake hataki kumpoteza mapema katika
tasnia hiyo.
Chidi
alisema, aliwahi kufanya kazi na Diamond kama mdogo wake hapo zamani wakati
Dimond anaanza muziki na alimwambia kwamba hatumii vitu hivyo amemtaka aendelee
hivyo.
“Diamond
ni mdogo wangu sana, nilishirikiana naye katika wimbo wake wa ‘Nalia’ wakati
ndio anaanza, na juzi kanisaidia sana katika wimbo wangu mpya kagharamia kila
kitu pia kanihaidi kugharamia video ya wimbo huo,” alisema.
Aidha,
Chid ametambulisha ngoma yake mpya inayojulikana kwa jina la ‘Mpaka kuchee’
ambayo ameshirikina na nyota wa muziki huo, Diamond, AY na Dully Sykes.
Alisema
wimbo huo umetengenezwa na watayarishaji wa muziki huo kutoka studio za Nyumba
ya Kukuza Vipaji Tanzania (THT), Emma The Boy na Tuddy Thomas.
No comments:
Post a Comment