HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 01, 2017

HAKUNA CHUKI NDANI YA LEBO YA WCB-Harmonize

Na Mwandishi Wetu

MSANII bongo fleva nchini, Rajab Ibrahim 'Harmonize' amesema kuwa hakuna ushindani wala chuki ndani ya lebo ya WCB tofauti na watu wanavyofikiria.

Akizungumza katika kipindi cha FNL cha EATV, Harmonize amesema ndani ya lebo yao hawajawahi kushindana wala wanapotoa nyimbo hawatoi kwa mashindano.

"Hakuna msanii wa lebo ya WCB anachukia pindi mwingine anapofanya kolabo na msanii mwingine mkubwa kwa kuwa kila mtu anakuwa na riziki na mafanikio yake," alisema.


Harmonize alieleza kuwa, "si kweli kama inavyodaiwa na baadhi ya watu kuwa tunaachia nyimbo kwa ajili ya kuzizima nyimbo za wasanii wengine...sisi tunapeana muda na kila mmoja ana muda wake wa kuachia nyimbo,".

No comments:

Post a Comment

Pages