Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandisi wa habari jijini Dar es Salaam leo, wakati akitangaza waimbaji waliodhibitisha kushiriki katika tamasha hilo. (Picha na Francis Dande).
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandisi wa habari jijini Dar es Salaam leo, wakati akitangaza waimbaji waliodhibitisha kushiriki katika tamasha hilo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandisi wa habari jijini Dar es Salaam leo, wakati akitangaza waimbaji waliodhibitisha kushiriki katika tamasha hilo.
NA MWANDISHI WETU
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandisi wa habari jijini Dar es Salaam leo, wakati akitangaza waimbaji waliodhibitisha kushiriki katika tamasha hilo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandisi wa habari jijini Dar es Salaam leo, wakati akitangaza waimbaji waliodhibitisha kushiriki katika tamasha hilo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandisi wa habari jijini Dar es Salaam leo, wakati akitangaza waimbaji waliodhibitisha kushiriki katika tamasha hilo.
NA MWANDISHI WETU
WAIMBAJI wa muziki wa injili wamezidi kumiminika
kuthibitisha ushiriki wao katika Tamsha la Pasaka litakalozinduliwa April 16
katika Uwanja wa Uhuru, jiji Dar es Salaam kabla ya kuhamia mikoa mingine
mitano kuutangaza ufalme wa Mungu na malengo yake mengine ya uwepo wake.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa
Kamati ya maandalizi ya Tamasha hilo linalofanyika mara ya 17, Alex Msama,
alisema ni faraja kwao kuona waimbaji mahiri wakizidi kuthibitisha tukio hilo
litakalowaleta na nyota wa ndani na nje ya nchi.
Msama
amewataja waimbaji wengine wapya ni Goodluck Gosbert anayetamba na kibao cha
Ubarikiwe, John Lissu, Kwaya ya Ulyankulu, moja ya kwaya kongwe na maarufu iliyowahi kutamba na vyimbo nyingi
zenye ujumbe kamili wa neno la Mungu ukiwemo ‘Kwa viumbe Vyote’ unaotikisa hadi
sasa.
‘Tunashukuru
sana kwani waimbaji wamezidi kuthibitisha kuashiria kuwa maandalizi ndiyo
yameshika kasi na wapenzi na mashabiki wa muziki wa injili, wakae mkao wa
kupokea Baraka za Mungu kupitia ujumbe wa nyimbo,’ alisema Msama.
Alisema
katika uzinduzi wa tamasha hilo utakaofanyika Uwanja wa Uhuru, utakwenda
sambamba na uzinduzi wa albamu ya
Kinondoni Revival Kwaya pamoja na kazi albamu mpya ya malkia wa nyimbo za
injili nchini na Afrika Mashariki na Kati, Rose Muhando.
“Uzinduzi wa
Tamasha la Pasaka April 16 katika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam,
utakuwa wa aina yake kwa sababu kutakuwa na uzinduzi wa albamu mpya mbili; moja
ya Kinondoni Revival Kwaya na nyingine Ruthu ya Rose Muhando,” alisema Msama
aliyechangia kwa kiasi kikubwa kukuza muziki wa injili kupitia matamasha.
Kuhusu mikoa
ambayo Tamasha hilo litapita, Msama alisema baada ya kuzinduliwa jijini Dar es
Salaam, mashambulizi yatahamia mjini Dodoma, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na
kumaliza kazi hiyo mkoani Iringa kwa mwaka huu na kuwataka wadau wa muziki wa
injili kuwa tayari kupokea Baraka.
No comments:
Post a Comment