Mwenyekiti
wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha Pasaka, Alex Msama, akizungumzia maandalizi
ya tamasha hilo litakalofanyika Aprili 16 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es
Salaam. (Picha na Francis Dande).
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha Pasaka, Alex Msama, akizungumzia maandalizi ya tamasha hilo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha Pasaka, Alex Msama, akizungumzia maandalizi ya tamasha hilo litakalofanyika Aprili 16 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
NA MWANDISHI WETU
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha Pasaka, Alex Msama, akizungumzia maandalizi ya tamasha hilo litakalofanyika Aprili 16 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
NA MWANDISHI WETU
KAMATI ya Maandalizi ya
Tamasha la Pasaka chini ya mwenyekiti wake Alex Msama, limeanza kutaja waimbaji
wa nyimbo za injili watakaoshambulia ‘tamasha la mwaka huu.
Mwimbaji wa kwanza kutajwa na
Kamati hiyo katika mkutano wake na waandishi habari jijinin Dar es Salaam leo,
ni Jesca Honole maarufu kama ‘Jesca BM.’
Msama alisema jana kwamba,
mwimbaji huyo amepata bahati ya kipekee ya kuwa wa kwanza na kwamba wengine
watawekwa hadharani baada ya kupitishwa rasmi na Kamati.
“Tunamshukuru Mungu kwa
sababu maandalizi ya Tamasha letu la Pasaka ambalo safari hii linakuja
kitofauti zaidi, waimbaji wameanza kupitishwa, ikiwa ni hatua nzuri ya tukio
hili la kimataifa,” alisema Msama na kuongeza.
‘Mwimbaji aliyebahatika kuwa
wa kwanza kuthibitishwa ni Jesca Honoli maarufu kama ‘Jesca BM’, mmoja wa waimbaji mahiri kwa sasa.”
Alisema nguvu ya kuanza
kutangaza waimbaji watakaohudumu katika Tamasha hilo litakaloanzia Uwanja wa
Uhuru, jijini Dar es Salaam April 16, ni baada ya kupata kibali rasmi cha tukio
hilo.
Kuhusu kibali, Msama ametoa
shukrani kwa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kwa kutoa baraka kwa tukio hilo
la kimataifa ambalo litatikisa katika mikoa ipatayo mitano ya Tanzania bara.
Alisema, baada ya Tamasha
hilo kuzindiliwa April 16 katika Uwanja
wa Uhuru, jijini Dar es Salaam, litahamia Uwanja wa Jamhuri, mjini Dodoma kabla
ya kutua katika mikoa mingine mitatu.
Alisema mbali ya Tamasha hilo
kubeba malengo yake ya msingi yakiwamo ya kueneza neno la Mungu na kutumia
sehemu ya mapato kufariji makundi maalumu, safari hii litatumika kama jukwaa la
kumuombea nch Rais John Pombe Magufuli na nchi kwa ujumla.
Manufaa mengine ya Tamasha hilo linalofanyika
tangu mwaka 2000, ni kuweza kukuza muziki wa injili kiasi cha kuwa ajira kwa
vijana wenye vipaji.
No comments:
Post a Comment