HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 22, 2017

MAHAFALI YA KIDATO CHA SITA SEKONDARI YA CHANG'OMBE MAZOEZI YAFANA JIJINI DAR ES SALAAM

Mkuu wa Shule ya Sekondari Chang'ombe Mazoezi, Daina Matemu, akimuongoza kuelekea kwenye ukumbi wa mahafali, mgeni rasmi katika mahafali ya Kidato cha Sita ya shule hiyo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Universities Abroad Link, Tony Kabetha (kushoto), wakati wa mahafali hayo, yaliofanyika Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), jijini leo. Nyuma kulia ni Mwenyekiti Kamati ya Taaluma (PTA), Ibrahim Samatta. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)  
Kijana wa Skauti kutoka shule hiyo, akimvisha skafu Mgeni rasmi katika mahafali ya kidato cha sita, Mkurugenzi wa Kampuni ya Universities Abroad Link, Tony Kabetha, mara baada ya kuwasili kwenye ukumbi wa mahafali hayo. Anayeangalia ni Mkuu wa shule hiyo, Daina Matemu. 
Mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Universities Abroad Link, Tony Kabetha (wa pili kulia), akiwa na wageni mbalimbali kwenye meza kuu wakipiga makofi mara baada ya kuasili ukumbini.
Wahitimu wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Chang'ombe Mazoezi, wakiimba wimbo wa shule hiyo, mbele ya mgeni rasmi Mkurugenzi wa Kampuni ya Universities Abroad Link, Tony Kabetha, wakati wa mahafali yao leo jijini Dar es Salaam. 
Mkuu wa Shule ya Sekondari Chang'ombe Mazoezi, Daina Matemu, akizungumza wakati akitambulisha wageni mbalimbali kwenye meza kuu katika mahafali hayo.
Mgeni rasmi akiwa na wageni mbalimbali kwenye meza kuu wakimwombea mmoja wa wanafunzi aliyefariki wakati wakiwa kidato cha tano, wahitimu hayo. 
Wahitimu wa kidato cha sita wakimwombea mwenzao aliyefariki wakiwa kidato cha tano.
Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Chang'ombe Mazoezi, Hussein Chiumbi, akisoma taarifa ya shule hiyo katika mahafali hayo. 
Baadhi ya wahitimu wakicheza ngoma za Bongo Fleva, wakati walipokuwa wakionesha vipaji vyao.  
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Taaluma, Elly Mdundo, akitoa taarifa ya maendeleo ya taaluma kwa mgeni rasmi. 
Baadhi ya walimu wa shule hiyo, wakiwa katika mahafali hayo. 
Mhitimu wa kidato cha sita, Mansoor Mohamed akisoma risala ya wahitimu. Anayemsaidia ni mhitimu mwenzake, Hefsiba Nyangi.
Wahitimu wa kidato cha sita, Mansoor Mohamed na Hefsiba Nyangi wakimkabidhi risala ya wahitimu mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Universities Abroad Link, Tony Kabetha.
Baadhi ya wazazi, ndugu na jamaa za wahitimu wa kidato cha sita, wakiwa katika mahafali hayo. 
Baadhi ya wahitimu wakionesha mitindo ya mavazi yaliyobuniwa na shule hiyo. 
Baadhi ya wahitimu wakipita na mavazi yaliyobuniwa na shule hiyo. 
Baadhi ya wahitimu wakipita mbele ya mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Universities Abroad Link, Tony Kabetha na mavazi yaliyobuniwa na shule hiyo. 
Mkuu wa Shule ya Sekondari Chang'ombe Mazoezi, Daina Matemu, akizungumza wakati akimkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Taaluma (PTA), Ibrahim Samatta (kushoto), ili amkaribishe mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Universities Abroad Link, Tony Kabetha (katikati), azungumze na wahitimu hao.
Mwenyekiti wa Kamati ya Taaluma (PTA), Ibrahim Samatta, akizungumza katika mahafali hayo, wakati akimkaribisha mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Universities Abroad Link, Tony Kabetha (katikati), azungumze na wahitimu hao. 
Mgeni rasmi katika mahafali ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Chang'mbe Mazoezi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Universities Abroad Link, Tony Kabetha, akizungumza na wahitimu wakati wa mahafali hayo, yaliofanyika Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), jijini leo. Kushoto ni Mwenyekiti Kamati ya Taaluma (PTA), Ibrahim Samatta na kulia ni Mkuu wa shule hiyo, Daina Matemu.

No comments:

Post a Comment

Pages