Mkurugenzi
Mtendaji wa Mamalaka ya Maji Musoma, Mhandisi Said Gantala (kushoto) akitoka
kwenye ukumbi wa Balili Rock Resort
mjini Bunda baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuamuru kuwa akamatwe na ahojiwe
na TAKUKURU Januari 19, 2018. Kulia ni Kamanda wa TAKUKURU wa mkoa wa Mara, Alex Kuhanda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameamuru Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Mara kumkamata na kumuhoji Mkurugenzi Mtendani wa Mamlaka ya Maji Musoma (MUWASA) Mhandisi Gantala Said kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za mradi wa maji Bunda.
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameamuru Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Mara kumkamata na kumuhoji Mkurugenzi Mtendani wa Mamlaka ya Maji Musoma (MUWASA) Mhandisi Gantala Said kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za mradi wa maji Bunda.
Mbali na Mkurugenzi huyo pia TAKUKURU
inawashikilia wakandarasi wanaojenga mradi huo ambao ni Mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi ya Nyakirang'anyi Bw
Mauza Mmangi ambaye ndiye mkandarasi anajenga mradi huo unaotoa maji kutoka Ziwa Victoria kwenye eneo la Nyabehu hadi Bunda mjini.
Wengine waliokamatwa ni pamoja na
Mhasibu wa Kampuni ya Ujenzi ya Nyakirang'anyi Bw. Amon Gideon pamoja na
viongozi wa kampuni nyingine ya ujenzi ya Fortrss Bw. Juvenari Chirianga na
Ephraim Mpeko ambao nao walishiriki katika ujenzi wa mradi huo.
Waziri Mkuu amefikia uamuzi huo jana jioni (Ijumaa, Januari 19,
2018) baada ya Mkurugenzi huyo kushindwa kueleza sababu zilizosababisha mradi
wa maji Bunda kutokamilika pamoja na
Serikali kutoa fedha nyingi.
Akizungumza katika kikao maalumu cha kujadili changamoto za utekelezaji
wa miradi ya maji mkoani Mara, alichokiitisha mjini Bunda, Waziri Mkuu alisema
aliamua kuitisha kikao hicho baada ya kutoridhishwa na utekelezwaji wa miradi hiyo
hususan inayosimamiwa na MUWASA.
Alisema kwa sasa Serikali inatekeleza Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli
ya kumtua mama ndoo kichwani. Kampeni hiyo
inayolenga kuwaondolea wananchi tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji
safi na salama, hivyo itawachukulia hatua wote watakaokwamisha miradi ya maji.
Waziri
Mkuu amesema malengo ya kampeni hiyo ni kuwafikishia wananchi huduma ya maji
safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao.
Pia Waziri Mkuu aliagiza kupitiwa upya kwa mradi huo kwa sababu hafurahishwi na ujenzi wake.”
Kama Mkurugenzi wa MUWASA anasema mradi umekamilika kwa asilimia 98 sasa kwa
nini wananchi walalamikie kukosa huduma hiyo.”
Alisema Mkurugenzi huyo amekuwa akimlipa mkandarasi fedha kabla
ya kufanya kazi ambapo hadi sasa tayari mkandarasi anayejenga mradi huo
ameshalipwa zaidi ya sh. bilioni saba na mradi haujakamilika na wananchi
wanaendelea kutumia maji ambayo siyo salama.
Waziri Mkuu alisema viongozi hao wahojiwe na wakibainika
kuhusika na ubadhilifuu wa fedha za mradi huo, wachukuliwe hatua kali za
kisheria.”Serikali imedhamiria kuimarisha huduma za maji, hivyo hatuhitaji mtu
atakayeenda kinyume na mpango huo.”
Mradi wa kupeleka maji kwenye mji wa Bunda maji kutoka ziwa Victoria
katika eneo la Nyabeho ulisanifiwa mwaka 2006 na ulikuwa unatekelezwa kwa awamu
kulingana na upatikanaji wa fedha za maendeleo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara
Bw. Adam Malima aliagiza kufungwa na ofisi za MUWASA na kuwataka wafanyakazi wa
mamlaka hiyo kutoruhusiwa kuingia ofisini hadi hapo uchunguzi utakapokamilika.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMAMOSI, JANUARI 20, 2018.
No comments:
Post a Comment