Naibu
Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa, akizindua vitabu vinne
vinavyohusu masuala ya kilimo jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni
Mkurugenzi Mtendaji wa Repoa Donald Mmari na Mtafiti Repoa Lulu Qlan`g
(katikati). (Na Mpiga Picha Wetu).
Naibu
Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa, akizingumza katika hafla hiyo.
Mwenyekiti wa REPOA Dk. Donald Mmari akizungumza katika hafla hiyo.
NA MAKUBURI ALLY
SERIKALI imewaasa
vijana kuwekeza elimu zao katika katika sekta ya kilimo ili kuweza
kutatua changamoto ya ajira ambayo imekuwa ni kilio kwa vijana wengi
wakitanzania.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam katika
uzinduzi wa vitabu vinne vilivyoandaliwa na Taasisi ya Repoa inayojihusisha na
mambo ya utafiti ambavyo vimelenga maendeleo ya kilimo, Naibu Waziri wa Kilimo Innocent
Bashungwa alisema vijana wanatakiwa wabadilike na wasome alama za nyakati hasa
kutokana na mazao yaliyopo hapa nchini yanahitajika katika nchi za jirani
ikiwemo Msumbiji, Malawi na mpaka nchi za Ulaya.
“Wakulima wetu wamekuwa wakizalisha mazao bila kujua wanauza
wapi lakini ndani ya Serikali hadi sasa mtaona chini ya wizara ya kilimo kuna
idara ya masoko kwaajili ya timu ya kutafuta masoko,” alisema Bashungwa.
Aidha, Bashungwa alisema kuwa unaweza ukawa kijana si lazima
ukashike jembe unaweza ukaanzisha kampuni ambayo imejikita katika masoko ya
mazao ya wakulima wa hapa nchini na ikawa ajira kwako.
Katika vitabu ambavyo vimezinduliwa na Naibu Waziri vimelenga
kutoa elimu juu ya kilimo pamoja na umwagiliaji hasa kutokana na tafiti ambazo
walizifanya Repoa.
Moja ya vitabu hivyo kimeelezea Elimu na uzalishaji kwenye
kilimo Tanzania Vijijini, kimeandaliwa na Profesa Lucas Katera, kingine
kimeeleza Tathmini ya mfumo wa Kitaasisi wa maboresho wa Utumishi kwa Umma,
ambacho kimeandaliwa na Dk Jamal Msami, kingine kinazungumzia Mabadiliko ya
kitaasisi na vikwazo vya Ushindani kwenye Masoko, ambacho kimeandaliwa na Dk
Donald Mmari na kitabu ambacho kimezinguzia Sera za kilimo na jitihada za
Kupunguza Umasikini Tanzania ambacho kimeandaliwa na Profesa Paschal Mihyo.
Amazing! This blog looks just like my old one! It's on a entirely different subject but it has pretty much
ReplyDeletethe same layout and design. Superb choice of colors!