HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 22, 2014

Benki ya Exim kuendelea kupiga jeki maendeleo ya michezo nchini
 Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro, Amio T. Amio (kushoto) akisalimiana na wafanyakazi wa Benki ya Exim wakati wa Mbio za Riadha za Ngorongoro zilizofanyika kupiga vita ugonjwa wa Malaria. (Na Mpiga Picha Wetu)
 Mkurugenzi wa mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro Amio T. Amio (kushoto) akikabiziwa zawadi ya kava la tairi ya gari kutoka kwa Ofisa Mauzo wa Benki ya Exim tawi la Karatu Nectae Exaud wakati wa Mbio za Riadha za Ngorongoro zilizofanyika kupiga vita ugonjwa wa Malaria.
 Mratibu - Ufundi wa Mbio za Riadha za Ngorongoro wa kwanza kulia  Filbert Bayi akitoa maelezo kwa wakimbiaji. Wa kwanza kushoto aliyevaa miwani ni Meneja wa Benki ya Exim tawi la Karatu  Emmanuel  A. Mwamkinga. Mbio hizo zilifanyika kupiga vita ugonjwa wa Malaria nchini.
 Wafanyakazi wa Benki ya Exim wakiwa na medali zao baada ya kukabiziwa medali hizo wakati wa Mbio za Riadha za Ngorongoro zilizofanyika kupiga vita ugonjwa wa Malaria.
Wafanyakazi wa Benki ya Exim wakiwa na medali zao baada ya kukabidhiwa medali hizo wakati wa Mbio za Riadha za Ngorongoro zilizofanyika kupiga vita ugonjwa wa Malaria. 

Na Mwandishi Wetu, Karatu

Benki ya Exim imejikita katika kusaidia maendeleo ya michezo nchini hususani mchezo wa riadha, ambao kwa siku za nyuma umekuwa ukipeperusha bendera ya Tanzania dhidi ya mataifa mengine ipasavyo katika mashindano ya kimataifa.

Ikiwa ni Benki ya sita kwa ukubwa Tanzania kwa upande wa mali na amana zake, Benki ya Exim imesema kwamba inataka kuwa sehemu ya mkakati wa heshima hiyo iliyopotea, ambapo imeanza kuingiza misaada yake katika michezo ya ngazi za chini ili kugundua vipajivilivyojificha na kuweza kuvitumia.

Akizungumza wakati wa mbio za riadha za Ngorongoro zilizoandaliwa na Zara Tanzania Adventures mwishoni mwa wiki mkoani Kilimanjaro, Meneja wa Benki ya Exim Tawi la Karatu, Bw. Emmanuel Mwamkinga alisema kuwa kuunga mkono miradi mbali mbali ya kijamii nchini ni moja kati ya shughuli za kijamii zinazofanywa na Benki ya Exim. 

“Mbio hizi zitawezesha vipaji vyetu katika ngazi ya chini kabisa kuonekana ambavyo upaswa kutumika ili kushiriki katika mashindano ya kimataifa. Mpaka sasa kuna wasiwasi kuwa kwa nini wanariadha wa kitanzania wanashindwa kuleta medali nyumbani, kinyume na ilivyo zamani. Kwa hivyo hii ni fursa ya kipekee kwa Chama cha Riadha nchini kutambua wanariadha wazuri na kuwaandaa vizuri ili waweze kuiwakilisha nchi kikamilifu,” alisema.

Bw. Mwamkinga alibainisha kuwa benki yake, kupitia tawi lake la Karatu imeungana na wadhamini wengine kupiga jeki mbio hizo ambazo lengo lake ni kuunga mkono jitihada za serikali za kukuza uelewa dhidi ya ugonjwa wa malaria, na kutokana mbio hizo vipaji vipya katika riadha vitagundulika.

Pia alisema kuwa udhamini huo ni moja kati ya mipango ya benki ikiwa inaangalia uwezekano wa kupanua huduma zake mkoani Kilimanjarona kwamba itakuwa ni fursa nzuri kwa benki kukuza jina lake.

"Benki ya Exim inajivunia kudhamini mbio hizi za Ngorongoro na kujiusisha nazo ambayo ni njia nzuri kwa watu kuifahamu benki ya Exim vizuri na ni fursa ya kujiinua kibiashara.

"Ngorongoro Marathon ni tukio ambalo linaumuhimu mkubwa katika kuitangaza Tanzania katika nyanja nyingi hasa uwezo mkubwa wa kiuchumi wakati pia utoa fursa kwa wanariadha wanaochipukia na wapya kupatikana,” Bw. Mwamkinga alisema.

No comments:

Post a Comment

Pages