HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 22, 2014

KITAMBI NOMA BINGWA BONANZA LA PASAKA  ARUSHA

Mwandishi Wetu Arusha

KITAMBI noma mabingwa wa jumla wa bonanza la Pasaka lililofanyika katika uwanja wa kumbukumbu ya sheikh Amri Kaluta Abeid huku timu ya Mango Garden ya Kinondoni ikishika nafasi ya pili ikiwa ni katika kusherehekea sikukuu ya pasaka kwa michezo mbalimbali.

Bonanza hilo lililoandaliwa na Klabu ya Kitambi noma yenye maskani yake jijini hapa na kufadhiliwa na kampuni ya bia (TBL)liliwakusanya mamia ya wapenda michezo na kushudia michezo ya kukimbiza kuku,kukimbia na magunia,soka,Kunywa bia,kuvuta kamba na burudani ya muziki kwa siku nzima ya pasaka.

Akifungua bonanza hilo Mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga al;iwataka washiriki wa bonanza hilo kufahamu kuwa michezo ni afya na burudani na tunatarajia kuona burudani kutoka kwenu kwani pia nimefarijika kuwaona marafiki zangu ambao wengine walikuwa wakicheza ligi kuu lakini kwa sasa vitambi vimewanyemelea hivyo michezo ni fursa nzuri ya kuvipunguza.

Makunga akawaka washiriki na watanzania kushiriki katika michezo baada ya shughuli zao katika suala zima la kujenga Afya zao na kuleta burudani hakika taswira hiyo itajenga taifa la watu wenye Afya na kuondoa magonjwa mbalimbali yanayoinyemelea jamii yetu.

Timu zilizoshiriki katika bonanza hilo ni pamoja na Arusha Coaches,kampuni ya Benson,Mango Garden ambao walikuwa wageni waalikwa kutoka jijini Dar es salaam na wenyeji Timu ya Kitambi Noma  zote za jijini Arusha ambapo katika soka timu zote zilicheza kwa mzunguko na kujikusanyia pointi na bingwa kupatikana.

Katika mechi ya kwanza kati ya Arusha coaches walifungwa bao moja bila majibu na timu ya mango garden ikifuatiwa na mechi ya wenyeji kitambi noma na timu ya bensons na kujikuta benson wakipigiliwa kwa bao mbili bila majibu mechi iliyofuata ni kati ya  timu ya makocha wa mkoa wa Arusha na Benson mchezo ulioisha kwa Arusha Coaches kuwapigilia bila huruma benson kwa bao 3 bila majibu.

Kwenye mchezo wa kuvuta kamba timu ya kitambi noma iliibuka mshindi katika fainali yake na timu ya benson huku benson na kitambi noma wakiibuka washindi kwa kugawana kuku moja moja katika mashindano ya kukimbiza kuku huku bonanza hilo likifana na kuwapa burudani murua wakazi wa jiji hili na viunga wake.

No comments:

Post a Comment

Pages