HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 30, 2014

DUDU BAYA AWASHAURI ALIKIBA, DIAMOND PLATINUMZ


 NA ELIZABETH JOHN

MKONGWE wa muziki wa kizazi kipya nchini, Dudu Baya amewataka wasanii wa muziki huo, Alikiba na Diamond Platinum kutumia vipaji vyao kutengeneza hela na sio kugombana.

Kauli hiyo ya Dudu Baya imekuja baada ya wasanii hao kuonekana wanaugomvi mkubwa ambao kila mmoja anauelezea kwa jinsi anavyoujua.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Dudu Baya alisema hao ni wasanii wenye vipaji na wanasoko kubwa katika tasnia hiyo hivyo ni vizuri wakichukua nafasi hiyo kutengeneza hela na sio kugombana.

“Hawa ni wadogo zangu mimi nawashauri tu, wakae chini wajitambue wao ni wakina nani wafikirie kutengeneza hela na sio kugombana kila siku,” alisema.

Dudu Baya ni msanii ambaye alitamba kipindi cha nyuma na ngoma yake ya ‘Nakupenda mpenzi’ ambayo ilifanya vizuri na kumtambulisha vema katika soko la muziki huo.

No comments:

Post a Comment

Pages