HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 25, 2014

MAALIM SEIF ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA POLISI

 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akiwasalimia maafisa wa Polisi Makamo Makuu ya Polisi Zanzibar.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akiwa katika picha ya Pamoja na Maafisa wa Polisi Ziwani Zanzibar.

Na Hamis Haji, Zanzibar
 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Maalim Seif Sharifa Hamad ametoa wito kwa Jeshi la Polisi Zanzibar kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maadili ya kazi na kuhakikisha askari hawafanyi kazi kwa misingi ya upendeleo, chuki, rushwa, wala ubaguzi wa aina yoyote.

Maalim Seif ameyasema hayo leo wakati alipotembelea Makao Makuu wa Polisi Zanzibar Ziwani, na kuzungumza na Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Makame pamoja na maafisa wa Jeshi hilo.

Makamu wa Kwanza amesema kwa kiasi kikubwa Polisi Zanzibar limepata mafanikio makubwa katika kusimamia majukumu yake, hasa ya kupunguza matendo ya uhalifu, lakini wapo miongoni mwa askari hujihusisha na matendo yaliyo kinyume cha maadili yanayolitia doa jeshi hilo.

Alisema zipo taarifa kwamba baadhi ya Maafisa wa polisi huvujisha taarifa na kuwapa watuhumiwa wa dawa za kulevya, pale jeshi hilo linapojiandaa kuwakamata na kuwafikisha mbele ya sheria.

Maalim Seif amesema tabia hiyo haina budi kukomeshwa kwa nguvu zote kwa sababu hudhorotesha mikakati ya kukomesha uingizwaji na biashara ya dawa za kulevya katika visiwa vya Zanzibar. 

Makamu wa Kwanza wa Rais amesema dawa za kulevya zinasababisha madhara makubwa kwa wananchi hasa vijana, na Polisi wanatakiwa kuwa mstari wa mbele katika kudhibiti uingizwaji wake kwa kushirikiana na taasisi za Kitaifa na Kimataifa.
“Nasikia baadhi ya wakati taarifa huvujishwa na maafisa wa Polisi. Kitengo cha Polizi cha Dawa za Kulevya lazima kiwe na watu waaminifu sana, Kamishna hili ni tatizo kubwa lazima tulikomeshe”, alisema Maalim Seif.   

Amelipongeza Jeshi hilo kwa juhudi kubwa linazozichukua kuwakamata watuhumiwa wa dawa za kulevya na kuwafikisha mbele ya sheria, lakini hata hivyo amesema bado juhudi zaidi zinahitajika kuwamata wafanyabiashara wakubwa ambao mara nyingi hawapatikanwi.

No comments:

Post a Comment

Pages