HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 26, 2014

KOZI YA WAAMUZI NA MAKOCHA YA COPA COCA-COLA YAANZA DAR

Mkufunzi wa FIFA Felix Tangawarima akizungumza wakati wa ufunguzi wa kozi ya waamuzi na makocha ya Copa Coca-Cola iliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. (Na Mpiga Picha Wetu)
 
NA SARAPIA JUSTINE

MKUFUNZI wa waamuzi kutoka Shirikisho la Soka Duniani  FIFA,  Felix Tangawarima kutoka Zimbabwe amesema jijini  Dar es Salaam kuwa programu ya waamuzi chipukizi wa mpira wa miguu Tanzania ni mfano wa kuigwa na nchi nyingine barani Afrika.

“Kwa jinsi nilivyoona, programu ya waamuzi chipukizi hapa Tanzania imepiga hatua kubwa kwa kuwa na vijana wengi wenye uelewa mkubwa kuhusu masuala ya uamuzi wa mpira wa miguu tofauti za nchi nyingine”, alisema Tangawarima wakati wa ufunguzi wa kozi ya waamuzi na makocha wa Copa Coca-Cola.

Tangawarima aliungwa mkono na mkufunzi mwingine wa FIFA Ulric Mathiott kutoka Seychelles ambaye anaendesha kozi hiyo ya siku tano kwa upande wa makocha. Mashindano ya Copa Coca-Cola yatafanyika mwezi ujao katika ngazi ya mkoa na Taifa.

Katibu Mkuu wa Shiriksho la Soka Tanzania (TFF) Selestine Mwesigwa na Mkurugenzi wa Ufundi Salum Madadi wamewataka makocha na waamuzi hao vijana kufuatilia kwa makini semina hiyo inayoendeshwa kwa nadhalia na vitendo. “Ni matarajio yetu kwamba mtaitumia semina hii kuboresha viwango vyenu vya ukocha na uamuzi na hatimaye kuboresha mashindano ya Copa Coca-Cola”, alisema Mwesigwa.

Kwa upande wake, Meneja Bidhaa wa Coca-Cola Tanzania Maurice Njowoka amewashukuru wakufunzi wa FIFA kwa kuja kutoa mafunzo na kusisitiza nia thabiti ya Coca-Cola kuendelea kushirikiana na TFF na wadau wengine wa soka nchini kuendeleza mchezo huo hapa nchini.
    
Washiriki wa semina hiyo ni Ahamed Simba kutoka Mwanza, Ali Kagile (Kagera) Alloyce Mayombo (Pwani), Andrew Zoma (Tabora), Anthon Mwamulima (Mbeya), Athman Kairo (Morogoro), Bakati Ali (Pemba Kaskazini), Charles Mayaya (Shinyanga), Fidelis Kalinga (Iringa) na Gabriel Gunda (Singida).

Wengine ni Hafidh Mucha (Pemba Kusini), Hamis Mabo (Kigoma), John William (Geita), Joseph Asey (Shinyanga), Joseph Haley (Manyara), Jumanne Mtambi (Kilimanjaro) Lenard Jima (Ruvuma), Madenge Omari (Mara), Mohamed Muya (Dodoma), Nicholous Kiondo (Ilala) na Nurdin Gogola (Temeke).

Wengine ni Osuri Kosuli (Simiyu), Peter Amas (Arusha), Ramadhan Ramadhan (Mjini Magharibi), Renatus Mayunga (Kinondoni), Samwel Moja, (Lindi), Safe Bakari (Katavi), Shaweji Nawanda (Mtwara), Heha Rashid (Unguja North) Tigana Lukinjo (Njombe), Yusuf Hamis (Unguja Kusini), Zahor Mohamed (Tanga) and Zacharia Mgambwa (Rukwa).

No comments:

Post a Comment

Pages