HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 19, 2014

KATIBA MBOVU CHANZO CHA MIGOGORO YA ARDHI

Na Mwandishi Wetu

MIGOGORO ya kupigania ardhi kati ya Wakulima na Wafugaji katika maeneo mbalimbali nchini inatokana na Katiba mbovu iliyopo sasa.

Kauli hiyo ilitolewa na mmoja wa Wakazi wa Kiteto mkoani Manyara, Ole Nkoko wakati alipozungumza kwa njia ya simu kuhusu mapigano yanayojitokeza mara kwa mara katika jamii hizo.

“Kama hakutapatikana Katiba inayotambua haki za wafugaji kama ilivyo kwa Wakulima wote bila ya kubagua wakubwa na wadogo basi serikali itambue migogoro hii itaendelea hata katika miaka 50 ijayo,”alisema Ole Nkoko.

Alisema Katiba hiyo inazuia kutengwa kwa maeneo ya wafugaji na baadala yake wafugaji wamekuwa wakipoteza ardhi na hivyokutishia uwepo wa ufugaji nchini. 

Ole Nkoko, alisema kutokana na mazingira hayo serikali imekuwa ikiwanyang’anya wafugaji maeneo yao kwa ajili ya utanuzi wa hifadhi ya wanyama pori, kilimo cha mashamba makubwa, utanuzi wa miundo mbinu ya majeshi ya ulinzi na usalama.

“Pia kuna visingizio vingi vinavyotolewa na baadhi ya viongozi kuwa wafugaji wanaharibu mazingira, hili  halina ukweli,”alisema Ole Nkoko.

Ole Nkoko, alisema kama wananchi watakumbuka, serikali iliwahi kutenga maeneo maalum ya mashamba kwa ajili ya mazao kama pamba, kahawa, tumbaku na katani lakini cha kushangaza  haijawahi kutenga maeneo kama hayo kwa ajil ya mifugo hali ambayo inachangia  wafugaji hao wanaponyang’anywa maeneo yao kusambaa wakitafuta malisho.

 “Tumetenga hata maeneo malum kwa ajil ya pundamila (hifadhi za taifa), lakini wafugaji wananing’inia hewani tu,”alisema hiyo ni kauli ya Mwalimu Nyerere, aliyoitoa Morogoro, mwaka 1981.

Ole Nkoko alisema sasa wafugaji wamekuwa kama watoto yatima wakihangaika huku na kule kwa ajili yakutafuta malisho ya mifugo yao ambapo wakati mwingine huzusha migogoro na wakulima.

Akizungumzia mgogoro wa Kiteto, Ole Nkoko, alisema mgogoro huo unaonekana ufumbuzi wake uko mbali kutokna na viongozi kutoonesha utashi wa kuumaliza na kuendelea kwake huenda ukawa na maslahi binafsi ya viongozi hao kisiasa.

Alisema kwa mfano mwaka huu viongozi mbalimbali akiwemo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na  Katibu Mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Abrahamani Kinana walitembelea eneo hilo huku wakishindwa kuupatia ufumbuzi zaidi ya kutoa ahadi ya kutafuta suluhu bila mafanikio.

Inadaiwa tangu kuibuka mgogoro huo Januari mwaka huu zaidi ya watu 30 wameuawa na wengine 200 kujeruhiwa.

No comments:

Post a Comment

Pages