Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Sabasaba Moshingi akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa mpango maalum wa kutoa mikopo kwa wastaafu
wa NSSF unaojulikana kwa jina la Wastaafu Loan.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la
Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Crescentius Magori akizungumza wakati wa uzinduzi wa
mikopo kwa wanachama wastaafu wa NSSF 'Wastaafu Loan' jijini Dar es Salaam.
Meza Kuu.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.
Wadau wakiwa meza Kuu.
Baadhi ya maofisa wa Benki ya Posta wakiwa katika hafla hiyo.
Meza Kuu.
Picha ya Pamoja.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Sabasaba
Moshingi (kulia) akibadilishana
mkataba wa mikopo na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la
Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Crescentius Magori kwa wanachama wastaafu wa NSSF jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la
Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Crescentius Magori (kushoto) akibadilishana
mkataba na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Sabasaba
Moshingi wa mikopo kwa wanachama wastaafu wa NSSF jijini Dar es Salaam
jana. (Picha na Francis Dande)
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Sabasaba
Moshingi (kulia) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NSSF, Crescentius Magori.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Sabasaba
Moshingi (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NSSF, Crescentius Magori.
Na Mwandishi Wetu
BENKI ya Posta Tanzania (TPB) kwa kushirikiana na Mfuko wa
Pensheni wa NSSF wamezindua mpango maalum wa kutoa mikopo kwa wastaafu
unaojulikana kama kwa jina la Wastaafu Loan.
Akizungumza na Waandishi wa habari leo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa
Shirika hilo Sabasaba Moshingi ,alisema lengo la mkopo huo ni kuwawezesha
wastaafu kukidhi mahitaji halisi ya fedha na kuboresha maisha yao.
Alisema kwa muda mrefu taasisi mbalimbali za fedha zimekuwa
hazitoi mikopo kwa wastaafu kwa kufikiria kuwa
hawana uwezo wa kulipa na kuwajengea dhana ya kutokopesheka.
“Kwa kuliona hilo na kutambua mchango wa wastaafu kwa taifa
hili,TPB kwa kushirkiana na Shirika la taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF)
wamebuni mpango huu wa kipekee nchini wa kuwakopesha wastaafu wa mfuko wa
NSSF,alisema.
Moshingi alisema kuwa utafiti uliofanywa umeonesha kuwa
wastaafu kwa ujumla wanaingiza kiasi kikubwa cha fedha katika kuleta athari
chanya katika nyanja mbalimbali za kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuongeza uwezo
wa kifedha katika taasisi za kifedha ,kuongeza ajira ,kukuza kipato kama fedha
hizo wakizitumia vizuri.
Mkurugenzi uendeshaji wa Mfuko wa NSSF Crescentius Magori alisema mkopo huo ni wa kwanza na wa
aina yake katika soko la mabenki hapa
nchini na kwamba utampa amani mwanachama wa NSSF ambaye amestaafu.
“Nina amini kwamba mkopo huu utamfanya mstaafu kuendelea na
maisha ya kawaida bila kuwa na hofu au wasi wasi kuhusu changamoto mbalimbali
atakazo kutana nazo katika maisha ya
kila siku,”alisema Magori.
Pia aliongeza kuwa mikopo hiyo imeanza kutolewa rasmi jana
(leo) katika matawi yote ya benki ya TPB na kwamba mstaafu atakayetaka kukopa
hatahitajika kuwa na dhamana ,na kwamba una bima .
Alifafanua pia kwa mstaafu anayetaka kukopa anatakiwa
kwenda tawi lolote la benki hiyo lililopo karibu kwa ajili ya kupata huduma za
haraka na bora.
“Na sasa wataweza
kunufaika na huduma za kimtandao kwa kuendelea kupokea pensheni zao kupitia benki yetu,na
kwa kufanya hivyo watssfu hawatalazimika kwenda benki kupanga foleni ili wapate
fedha zao,”alisema Magori.
No comments:
Post a Comment