HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 11, 2015

BENKI YA CRDB YAPATA FAIDA YA BILIONI 95.6

Na Pamela Mollel, Arusha

Benki ya CRDB imepata faidi yazaidi ya shilingi bilioni 95.6 sawa na asilimia 14 kwa mwaka 2014 ambapo ongezeko hilo ni kubwa ukilinganisha na faida ya miaka ya nyuma ambapo hali hiyo imesababishwa na uboreshwaji wa mfumo wa utaoaji pesa kwa wateja wao.

Hayo yameelezwa na mkurugenzi mkuu wa Benki hiyo Dk.Charles Kimei wakati akiwasilisha taarifa ya bodi ya wakurugenzi katika mkutano wa 20 wa wanahisa wa benki hiyo jijiji Arusha.

Dk. Kimei alisema kuwa kufwatia faida hiyo benki hiyo itatoa gawiola shilingi 15 kwa kila hisa moja ya mwanahisa kwa mwaka huu ikiwa na lengo la kuwanufaisha wanahisahao nakuongezea faida ya hisa zao.

Hata hivyo  Benki hiyo iko katika mchakato wa kuweza kuongeza mtaji wa banki hiyo ili kuweza udhibiti wizi wa pesa kwenye mtandao na kuboresha mifumo ya utoaji na kuweka pesa katika banki hiyo na kuweza kuwahhakikishia usalama wa pesa zao .

Dk. Kimei aliongeza kuwa katika uboreshaji wa huduma ya benki hiyo wameweza kuongeza  mawakala 575 wa fahari huduma  na mashine za Atm 375 nchi nzima ili kuweza kuwarahishishia wateja wao kupata huduma za kibenki pindi wanapohitaji.

Kwa upande wake mmoja wa wanahisa Bw,Rashidi Materuka alisema kuwa nimmoja wa mnufaikaji wa hisa ambae anakopa fedha kuputia banki hiyo shughuli za  kilimo na zimeweza kumkwamua katika kupambana na adui umaskini katika kilimo.
Aliongeza kuwa kutokana na kunufaika na huduma za banki hiyo anatkuwa chachu ya mabadiliko kwa wakulima wenzake katika eneo analotoka.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akizungumza katika mkutano wa 20 wa wanahisa wa benki hiyo uliofanyika Arusha,Tanzania.
Katibu wa Benki ya CRDB, John Rugambo akiwa katika mkutano huo.
 Mwenyekitiwa Bodi Martin Mmari akizungumza wakati wa mkutano huo.
Naibu Mkurugezi Mtendaji waBenki ya CRDB Huduma Shirikishi, Esther Kitoka akifuatilia mkutano wa 20wa wanahisa wa benki hiyo.
Wakurugenzi wa benki ya CRDB wakiwa katika mkutano huo.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyopadhyay akiwa katika mkutano huo.
 Wanahisa wakiwa katika mkutano huo.
Wanahisa.
Baadhi ya maofisa wa benki ya CRDB wakiwa katika mkutano huo.
Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye akiwa katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Martin Mmari akimkabidhi tuzo ya uongozi uliotukuka katika benki ya CRDB aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu wa benki hiyo kwa kipindi cha miaka 15, Damian Ruhinda, makabidhiano hayo yalifanyika wakati wa mkutano mkuu wa 20 wa wanahisa wa benki hiyo uliofanyika katika ukumbi wa AICC jijini Arusha, mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Dk. Charles Kimei.
Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Dk. Charles Kimei akimpongeza, HamisKananda aliyepokea tuzo ya uongozi uliotukuka katika benki ya CRDB aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu wa benki hiyo kwa kipindi cha miaka 15, mama Gatty Marwa. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi, Martin Mmari.
Mwenyekiti wa Bodi, Martin Mmari (katikati) akimkabidhi tuzo, Hamis Kananda aliyepokea tuzo ya uongozi uliotukuka katika benki ya CRDB kwa niaba ya aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu wa benki hiyo kwa kipindi cha miaka 15, mama Gatty Marwa.  Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Dk. Charles Kimei.
Wanahisa.
wanahisa wakiwa katika mkutano huo.
Mwanahisa ambaye pia ni mtangazaji nguli, Salim Mbonde akiuliza swali katika mkutano huo.
Mwanahisa akipiga kura kuchagua wakurugenzi wa bodi CRDB.
Mwanahisa akipiga kura kuchagua wakurugenzi wa bodi CRDB kuziba nafasi za waliomaliza muda wao.
Msanii Chief Omary Mwaliko akimkabidhi ramani ya Afrika, Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu wa 20 wa Benki ya CRDB.
Wanahisa wakiwa katika mkutano huo.
Wanahisa wakifuatilia mkutano huo.
Mkurugenzi wa Masoko Utafiti, Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (kulia) akiwa katika mkutano huo.
Mkurugenzi wa Masoko Utafiti, Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (kushoto) akijadiliana jambo na maofisa wa benki hiyo.





No comments:

Post a Comment

Pages