HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 23, 2015

DIAMOND AOMBA SAPOTI YA SERIKALI

NA ELIZABETH JOHN

MSHINDI wa tuzo ya mtumbuizaji bora wa kiume Afrika (Mtv MAMA 2015), Nassib Abdul ‘Diamond Platnumz’ ameiomba serikali kumpa sapoti katika kazi nzuri anayoifanya kutokana na kuitangaza vyema Tanzania katika mataifa mbalimbali.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Diamond alisema kuwa, licha ya kuleta tuzo hiyo nyumbani kwa mara ya kwanza hajaona sapoti yeyote iliyooneshwa na serikali au Baraza la Sanaa la Taifa (Basata).

Diamond alisema kuwa tuzo aliyoileta nyumbani ni kubwa hasa ukiangalia hakuna msanii yeyote ambaye alifanikiwa kuipata hivyo alihitaji sapoti kutoka kwa serikali au Basata kutokana na kazi hiyo nzuri ambayo imezidi kumjenga Kimataifa.

“Kiukweli nasapotiwa na watanzania ila sio serikali kwa sababu napata pongezi kutoka kwa kila mmoja kwa nafasi yake, ingekuwa vizuri kama mkutano huu wa kuwashukuru Watanzania wangeifanya serikali na sio uongozi wangu hivyo nawashauri Basata wawe wanatusapoti na sisi tunaofanya vizuri na sio kuangalia nani kakosea,” alisema Diamond.

Nyota huyo aliwashukuru Watanzania kwa kumsapoti kufanikisha kutwaa tuzo hiyo ambayo anakiri imezidi kumpa fursa ya kutamba Kimataifa ambapo baada ya kufanya kutumbuiza katika hafla ya utoaji tuzo hizo zilizofanyika Julai 18 huko Durban, Afrika Kusini mwanamuziki kutoka Marekani Neyo, aliomba kufanya naye kolabo.

Diamond alisema kwamba changamoto anayokutana nayo katika muziki wake ni ugumu wa soko la muziki wake, kwamba anapotaka kutoa kazi lazima aumize kichwa kutambua mashabiki wake wanamsapoti kazi ya aina gani.

No comments:

Post a Comment

Pages