HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 04, 2016

Sunshine Gypsum kuja na mikakati ya kuondoa tatizo la umeme viwandani

John Wang,  Meneja Masoko wa kampuni ya Sunshine Gypsum Limited ya Kibaha mkoani Pwani, akionyesha vipande vya gypsum vinavyotengenezwa na kampuni yake.  John Wang alikuwa akizungumza na waandishi wa habari juu  ya umuhimu wa umeme katika manendeleo ya  sekta ya viwanda hapa Tanzania. 

Na  Mwandishi  Wetu

Kuimarika  sekta  ya Umeme ni ukombozi pekee  wa maendeleo ya viwanda  katika kujenga uchumi  imara na endelevu nchini Tanzania.

Mwekezaji wa  kiwanda cha Sunshine Gypsum  Limited cha Kibaha mkoani Pwani, John Wang ametoa ushauri huo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

John Wang ambaye ni Meneja Masoko wa kiwanda hicho amesisitiza  kuwepo kwa  mikakati ya makusudi wa kuondoa  tatizo la umeme  linalokabili sekta ya  viwanda nchini Tanzania.

Amesema kuwa kwa sasa sekta ya  viwanda inaongezeka kwa kasi sana na kufanya uzalishaji kuwa mkubwa katika miaka  kumi inayokuja.

Licha ya kukiri kuwepo kwa mikakati ya kitaifa ya  kuimairisha sekta ya umeme, John Wang amesema  kuwa  kasi ya  mendeleo ya viwanda hapa Tanzania inaongezeka kwa kasi kubwa  kuliko mikakati hiyo.

Meneja Masoko huyo amedai kuwa serikali lazima itoa msukomo wa kutosha katika kuimarisha sekta hiyo ya viwanda inayozalisha bidhaa bora hapa Tanzania.

Amesema kuwa viwanda hapa Tanzania havina budi  kupata msaada  wa upendeleo hususani katika sekta nyeti hiyo ya umeme.

“ Kwa kweli umeme ni tatizo linalotakiwa kuangaliwa kwa macho ya serikali kwa sababu ni  msiba kwa wenye viwanda hapa nchini”, amesema John Wang

John Wang  pia maelalamikia tatizo la usafirishaji wa mali ghafi kutoka sehemu inakopatikana kwenda  eneo  la   kiwanda.
Amesema kuwa usafirishaji wa mali ghafi  ni eneo lingine linalotakiwa kuangaliwa kwa macho mawili  na serikali kwa sababu bidhaa zinacheleweshwa  kufika  eneo la viwanda  kwa sababu ya mfumo mbovu wa usafirishaji hapa nchini.

Kuhusu wafanyakazi wa kitanzania waliopo katika kiwanda cha Kibaha mkoani Pwani, John Wang amesema kuwa anatarajia kuwapa mafunzo zaidi  kwa wafanyakazi wake 100 wa kiwanda hicho.

Amesema kuwa anatarajia kuleta mitambo  ya kisasa  katika kiwanda chake na kufanya uzalishaji uongezeke  mara dufu katika mwaka 2016 hadi 2018.

No comments:

Post a Comment

Pages