HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 09, 2016

Wakazi 1500 kuathirika na Magonjwa ya Mlipuko, Malaria-Mwalazi

Zahanati isiyotumika kwa miaka 12 
 
Na Bryceson Mathias, Mwalazi Nyandira

WAKAZI 1,500 wa Kijiji cha Mwalazi, Kata ya Nyandira, Tarafa ya Mgeta, wako hatarini kuathirika na Magonjwa ya Mlipuko, Malaria, Vifo vya Watoto na Wajawazito, kutokana na Zahanati yao ya Kitongoji cha Mbigila kutofanya kazi kwa miaka 12.

Hayo yamesemwa na Wajawazito waliodai, wakiwa na Magonjwa ya Mlipuko, Uzazi na Malaria, hubebwa na Machela, Vitanda, Mizeganzega hadi Mgeta Kilomita Tano na Kibuko Kilomita Tatu kwa kupanda Mlima, huku maisha yao yakiwekwa rehani.

Wakizungumza na Wandishi siku ya akina Mama duniani jana,  Wajawazito walioomba wasitajwe wameilaumu Serikali Kuu na watendaji wakidai, Zahanati hiyo isipofunguliwa watakufa kwa Magonjwa hayo na Uzazi ikiwemo Degedege kwa watoto wadogo.

“Tukipata dharura za Uzazi usiku, tunakuwa hatarini hasa tunapobebwa na Machela, Vitanda au Mizeganzega, na mara kadhaa tunajifungulia njiani kutokana na umbali na ubovu wa miundo mbinu, hali ambayo ni hatari kiafya wanapotuhudumia.

“Adha hiyo pia inawasibu watoto wadogo hadi miaka mitano, wanaopata magonjwa ya kitoto likiwemo degedege na Magonjwa ya Kuhara! Na kijiji chetu cha Mwalazi, kinaongoza kwa Vifo kutokana na dharura hizo”.alisema mama mmoja mjamzito!

Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya, Dkt. Omari Mbena, alipoulizwa kwa njia ya simu ya kiganjani hakuwa na Majibu, na alipoambiwa anazungumza na mwandishi alikwepa maswali akiuliza eneo walipo wandishi! Na alipoandikiwa Ujumbe mfupi alidai,

“Ndugu yangu ungefika ofisini ili upate maelezo kamili ya zahanati hiyo maana naweza kukujibu tofauti”.alijibu Dkt. Mbena, huku wandishi wakihoji, kwa nini anataka waende ofisini badala ya eneo la tukio? 
 
Hata hivyo alitafutwa Diwani wa Kata ya Nyandira, Peter Zengwe, na kumbanwa aeleze kinachokwamisha kufunguliwa kwa zahanati hiyo ili iokoe Maisha ya Wananchi, Watoto na Nguvu kazi ya Taifa, ambapo alikiri malalamiko ya wakazi ni ya kweli na kudai,

“Zahanati hii ipo tangu enzi za Mkuu wa Wilaya, Sarah Linuma, imegharimu Mil. 26/- hadi sasa, ila kuna Siasa chafu zinafanywa isifunguliwe, ingawa imekamilika na Wananchi, Wajawazito na Watoto, wanaendelea kuteseka kwa kubebwa Machela na Mizeganzega, huku maisha yao yakiwa hatarini”.alisema Zengwe!

No comments:

Post a Comment

Pages