Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles
Mwijage amesema serikali ya Tanzania kupitia Ushirikiano wa Kimataifa wa Japani
(JICA) imejipanga kuboresha bidhaa zinazozalishwa chini ya kiwango.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar esa
salaam, Mwijage alisema serikali imeandaa mpango wa maendeleo wa miaka
mitano (FYDP II).
Alisema mfumo huo wa kuwekeza katika biashara kupitia
mfumo wa (Kaisen), ambao utasaidia kuboresha viwanda vikubwa na vidogo
vilivyopo nchini.
Mwijage alisema mfumo huo utawajengea
wafanyabiashara wa viwanda mazingira
mazuri ya kibiashara hivyo wawekezaji wajitokeze.
Alisema mfumo wa ‘Kaizen’ utasaidia kuboresha
rasilimali watu, kutengeneza bidhaa zenye viwango vya hali ya juu ambapo
tutakuwa tukizalisha kwa tija.
Kwa upande wake mwakilishi wa JICA, Toshio Nagase
alisema katika kukuza maendeleo ya viwanda kaizen itasaidia kubadilisha
mazingira ya biashara na ushauri katika sera ya viwanda.
Nagase alisema wanasaidia viwanda vidogo kupitia
maendeleo,mpango wa dhamana wa mikopo ya SIDO-CRDB,kuendeza viongozi kupitia
udhamini wa masomo pamoja na kozi mbalimbali za masomo.
No comments:
Post a Comment