HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 25, 2016

Dar mwenyeji maonesho ya Africa-PPB-EXPO Tanzania 2016

Dar es Salaam, 25, May 2016- Maonesho ya kwanza  ya bidhaa za plastiki, mpira, kemikali za petrol na ujenzi  yanatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Mlimani City jijini Dare s Salaam  kuanzia Mei 27 hadi 29 mwaka huu. Maonesho hayo ambalo yanajulikana kama Africa-PPB-EXPO Tanzania 2016, yatakuwa na washiriki na wageni kutoka  nchi zote za Afrika  Mashairiki na  Kati pamoja na mikutano ya B2B na fursa zinazohusiana.
 
Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Meneja Mkuu wa kampuni ya EXPO ONE ambayo ni waandaji wa maonesho hayo ya EXPO, Ahmed Barakat alisema kwamba maonesho ya  Africa-PPB-EXPO yatakuwa ni jukwaa la kipekee la maonesho ya bidhaa mpya na yanatoa mwanya wa kuyaelewa masoko yake ambayo  hayafahamiki vizuri.
 Africa-PPB-EXPO ni maonesho ya kimataifa ya bidhaa za plastiki, mipira, kemikali za petrol na ujenzi ya nchini Misri.
“Maonesho haya yamebuniwa ni  kukuza umoja miongoni mwa Waafrika kwa kuimarisha mahusiano ya kibiashara  kati ya Misri na Tanzania na hali kadhalika  kuyaweka masoko yake kwenye ramani ya Afrika,” alisema Barakat na kubainisha  kuwa Tanzania ni ya kwanza  katika orodha ya nchi za Afrika ambapo Africa-PBB-EXPO imepanga kushirikiana nayo.
Aramex Africa ni mshirika rasmi wa usafirishaji wa Africa-PBB-EXPO na itakwua inatoa mchango mkubwa katika kutoa huduma za ugavi na usafirishaji  kutoka Misri hadi Tanzania.
Kupitia Aramex na kwa uratibu wa TanTrade na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Africa-PBB-EXPO  inatoa fursa ya kipekee kwa waoneshaji  walio na kanzidata za kina kusajiliwa mara zinapopokelewa. Kanzidata hizo zinajumuisha hali ilivyo ndani ya soko la Tanzania na thamani yake pamoja na takwimu sahihi ya kuuza na kuagiza.  Hii inatoa  fursa ya uhakika kwa mikutano ya mkakati ya B2B pamoja na ufanisi unaohusiana pindi zinapofika.
  Meneja Mkuu huyo wa EXPO ONE alitoa wito kwa wafanya biashara kushiriki katika maonesho hayo ili waweze‘kubaini fursa za ushirikiano katika masoko haya mapya pamoja na mtandao ulio na wateja na wenza wa kibiashara.’  
“Kwa kushiriki katika maonesho ya Africa-PPB-EXPO, pamoja na mambo mengine washiriki watajifunza jinsi maudhui ya kina ya sekta yanaweza kuathiri biashara zao,  umoja uliopo miongoni mwa viongozi wa sekta, kupata washirika wapya na kulinganisha kiwango chao katika mitazamo ya ubunifu.
Kampuni ya EXPO ONE ambayo ni mwandaaji, ni taasisi ya kati ya  usimamizi wa mikutano na maonesho ambayo imejikita katika  kuandaa na kutoa huduma kwa maonesho ya  biashara ya kimataifa  pamoja na kuyatangaza mabanda ya Misri katika maonesho ya ndani na ya kimataifa.
Waandaaji wengine ni pamoja na Aramex, Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara, Baraza la Mauzo ya Mbolea na Kemikali, Chama cha Wazalishaji na Wauzaji wa Plastiki Misri (Epema) na Taasisi ya sekta Binafsi Tanzania (TPSF). Wengine ni Umoja wa sekta Binafsi Kenya, na  Chama cha Biashara Kimataifa China.
Maonesho mengine  ya Africa-PPB-EXPO yanatarajiwa kufanyika nchini Senegal na baadaye nchini Angola.

No comments:

Post a Comment

Pages