Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) linashiriki kwenye maonesho ya nanenane ambayo yanafanyika kitaifa katika viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Katika maonesho hayo NSSF inatoa huduma mbalimali zikiwemo kutoa taarifa za michango za wanachama, kuandikisha wanachama wapya na kutoa kadi mpya kwa wanachama wa zamani, kutoa maelezo juu ya uuzaji wa nyumba za mtoni kijichi phase 3 na Viwanja vya Kiluvya na pia kutoa elimu ya mafao na huduma mbalimbali zitolewazo na NSSF.
NSSF inapenda kuwakaribisha wananchi wa Lindi na Mtwara kutembelea banda lao lililopo kwenye viwanja hivyo vya Ngongo.
Afisa wa NSSF mkoa wa Lindi, Saad Juma akitoa maelezo kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi waliotembelea banda la NSSF kwenye maonesho ya Nanenane mkoani humo.
Afisa Matekelezo wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), mkoa wa Lindi, Adam Mbena akimwandikisha kujiunga na NSSF mmoja wa wakazi wa Lindi aliyetembelea kwenye maonesho ya Nanenane.
Afisa Mifumo ya Kompyuta Rukia Penza akimuelezea mwanachama taarifa yake ya Michango alipotembelea banda la NSSF kwenye maonesho ya nanenane Lindi
Afisa Masoko Muandamizi Amina Mmbaga akiwapa maelezo wakazi wa Lindi waliotembelea banda la NSSF kwenye maonesho ya nanenane anayoendelea mkoani Lindi.
Wakazi wa Mkoani Lindi wakiingia kwenye banda la NSSF ili kupata taarifa mbalambali kwenye maonesho ya nanenane yanayoendelea kwenye viwanda vya ngongo Mkoani Lindi.
Wakazi wa Mkoani Lindi wakiingia kwenye banda la NSSF ili kupata taarifa mbalambali kwenye maonesho ya nanenane yanayoendelea kwenye viwanda vya ngongo Mkoani Lindi.
No comments:
Post a Comment