HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 31, 2016

MAANDAMANO YA UKUTA YAAHIRISHWA

Mwenyekiti wa Chama cha demokrasia na Maendeleo (Chadema), akiongozana na Makamu Mwenyekiti cha Chadema, Zanzibar, Said Issa Mohamed wakiwasili katika mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam, leo, wakati wa kutoa tamko la kuahirishwa kwa maandamano ya UKUTA. (Picha na Francis Dande)
Waziri Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa akiwasili katika mkutano huo. Kushoto ni Mbunge wa Kibamba, John Mnyika.
Viongozi wa Chadema wakiwa wameshikana mikono kuonyesha mshiokamano wao wakati wa mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya Chama hicho jijini Dar es salaam, leo wakati wakitoa tamko la kuahairishwa kwa maandamano ya UKUTA.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya Chama hicho jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa zamani, Edward lowassa akipeana mkono na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe. Katikati ni Said Issa Mohamed ambaye ni Makamu Mwenyekiti Zanzibar.

 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akipeana mkono na mbunge wa Kibamba, John Mnyika.
 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya Chama hicho.
 Waziri Mkuu wa zamani, Edward lowassa ambaye pia na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa akizungumza katika mkutano huo.

Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo ametoa maadhimio ya Kamati Kuu ya chama hicho (CC), kuhusu kuahirishwa kwa uzinduzi wa Maandamano ya UKUTA hadi Oktoba Mosi ili kutoa nafasi kwa viongozi wa dini ili kukutana na Rais Dk. John Magufuli kwa maslahi ya Taifa.

Akitoa tamko la maamuzi ya Kikao cha Kamati Kuu (CC), mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema kuwa sababu kubwa zilizofanya kuahirisha kwa maandamano hayo ni kutoa nafasi kwa viongozi wa dini waliotaka kuahirishwa kwa uzinduzi wa maandamano hayo ili kutoa nafasi ya mazungumzo ya viongozi wa taasisi mbalimbali za dini na Rais John Magufuli.

Katika mkutano huo Mbowe alisema kuwa walikutana na taasisi za dini zikiwemo Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT), Makanisa ya Kipentekoste ya Karismatiki, Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) na Mufti Mkuu wa Zanzibar, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Baraza la Kikristo Tanzania (CCT) na Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT).

Pia walikutana na taasisi za kiraia kama Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Jukwaa la Wahariri (TEF), pamoja na Jukwaa la Katiba (JUKATA).

No comments:

Post a Comment

Pages