HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 27, 2016

WAZIRI PROFESA MBARAWA AZINDUA BODI YA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA JIJINI DAR ES SALAAM

Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania, Dk. Haruni Kondo.
 Mjumbe wa Bodi, Stella Nghambi.
Mjumbe wa Bodi, Dk. Jasson Kagonza.
 Mjumbe wa Bodi, Khadija Shaaban.
Mjumbe wa Bodi, Fatuma Bakari.
Mjumbe wa Bodi, Leonard Kitoka.
Mjumbe wa Bodi, Dk. Ubena John.
Katibu wa Bodi ya Shirika la Posta, Rochus Assenga.
Kaimu Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Fortunatus Kapinga, akizungumza kuhusu shirika hilo, kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Bodi, Dk. Haruni Kondo, kuzungumza wakati wa uzinduzi wa bodi mpya ya shirika hilo jijini Dar es Salaam leo.(Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Kaimu Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta, Fortunatus Kapinga, akizungumza kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya shirika, Dk. Haruni Kondo.
Mameneja wa Shirika la Posta Tanzania, wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa bodi mpya ya shirika hilo.
Baadhi ya wajumbe wa bodi mpya ya Shirika hilo, wakiwa katika uzinduzi wa bodi hiyo.
Baadhi ya wajumbe wa bodi mpya wakiwa katika uzinduzi wa bodi hiyo.
Meneja Mkazi Zanzibar wa shirika la Posta, Mwanaisha Saidi (katikati), Meneja wa Huduma za Barua, Fadya Zam (kulia) na Meneja Utumishi wa shirika, William Makumba (kushoto), wakiwa katika uzinduzi wa bodi hiyo.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia matukio mbalimbali katika uzinduzi wa bodi hiyo.
Baadhi ya viongozi wa Shirika la Posta wakiwa katika uzinduzi wa Bodi mpya ya Shirika hilo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania, Dk. Haruni Kondo, akitoa maelezo mafupi kuhusu bodi hiyo mpya pamoja na shirika hilo kwa jumla kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (katikati), kabla waziri Mbarawa hajaizindua rasmi bodi hiyo. Kushoto Ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo (Mawasiliano), Profesa Faustine Kamuzora.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, (Mawasiliano), Profesa Faustine Kamuzora, akitoa hutuba yake kabla ya kumkaribisha Waziri wa wizara hiyo, Profesa Makame Mbarawa (katikati), kutoa hotuba yake ya uzinduzi wa Bodi mpya ya Shirika la Posta Tanzania leo, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya viongozi wa Shirika la Posta wakinukuu hotuba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,Profesa Makame Mbarawa.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,Profesa Makame Mbarawa, akizungumza wakati alipoizindua rasmi bodi mpya ya Shirika la Posta Tanzania, leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa bodi hiyo, Dk. Haruni Kondo.
Baadhi ya wajumbe wa bodi ya Shirika la Posta wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,Profesa Makame Mbarawa, alipokuwa akitoa hotuba yake ya uzinduzi wa bodi hiyo, leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,Profesa Makame Mbarawa, akizungumza wakati akiizindua rasmi bodi mpya ya Shirika la Posta Tanzania, leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa bodi hiyo, Dk. Haruni Kondo.
Kaimu Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta, Fortunatus Kapinga (kushoto), akifuatilia hotuba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, wakati wa uzinduzi wa bodi mpya ya shirika hilo, leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,Profesa Makame Mbarawa (katikati), akikata utepe mkoba wa vitendea kazi kabla ya kumkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania, Dk. Haruni Kondo (kulia), wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, (Mawasiliano), Profesa Faustine Kamuzora.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (katikati), akimkabidhi vitendea kazi Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania, Dk. Haruni Kondo.
Mjumbe wa Bodi, Stella Nghambi, akitoa neno la shukurani baada ya Waziri Profesa Mbarawa kuizindua bodi hiyo.
Picha ya Pamoja ya Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (katikati waliokaa), mara baada ya kuizindua bodi hiyo leo jijini Dar es Salaam.  
Picha ya Pamoja ya viongozi wa Shirika la Posta na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kushoto waliokaa), mara baada ya kuizindua bodi hiyo leo jijini Dar es Salaam.  

No comments:

Post a Comment

Pages