HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 09, 2017

PROF. MBARAWA AUNDA TIMU YA WATAALAM UJENZI TERMINAL III

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akikagua Ujenzi wa Jengo la Tatu la Abiria (TB III), katika Uwanja cha Ndege wa Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, baada ya kuunda timu mpya ya kusimamia ujenzi huo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Salim Msangi. (Picha na Francis Dande).
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akitembelea Ujenzi wa Jengo la Tatu la Abiria (TB III), katika Uwanja cha Ndege wa Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, baada ya kuunda timu mpya ya kusimamia ujenzi huo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Salim Msangi na kushoto ni  Msimamizi wa Mradi wa Ujenzi, Ray Mciob. 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari, (hawapo pichani), mara baada ya kukagua ujenzi wa Jengo la tatu la Abiria (TB III), jijini Dar es Salaam. Picha na Kitengo  cha  Mawasiliano Serikalini, Wizara ya UJenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (kushoto), akitoa maelekezo kwa timu aliyoiteua kusimamia ujenzi wa Jengo la Tatu la Abiria (TB III), mara baada ya kuteuliwa leo jijini Dar es Salaam. 

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ameteua timu mpya ya wataalamu saba kwa ajili ya kusimamia mradi wa ujenzi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III), katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.
Hatua hiyo imefikiwa kufuatia agizo la Mheshimiwa Rais John Magufuli alilolitoa jana wakati alipofanya ziara ya kushtukiza uwanjani hapo  kujionea maendeleo yaliyofikiwa katika mradi huo.
Timu hiyo inaongozwa na Eng. Julius Ndyamukama inaundwa na  Eng, Godson Ngomuo, Eng. Humphrey Kanyenye, Eng. Abednego Lyanga, Eng. Mbila Mdemu na Eng. Rehema Myeya.
“Naamini timu hii ina wataalamu mahiri, hivyo itasimamia ujenzi huu kukamilika kwa wakati na kwa kuzingatia thamani ya fedha (value for money”, amesema Waziri Mbarawa.
Profesa Mbarawa amemhakikishia mkandarasi wa kampuni ya BAM kutoka uholanzi inayojenga jengo hilo kuwa Serikali itamlipa mkandarasi huyo katika kipindi cha wiki mbili kutoka sasa.
Aidha, ameitaka timu hiyo kuhakikisha ujenzi wa jengo hilo unakamilika mwezi Desemba mwaka huu kama ilivyopangwa.
Kwa upande wake Meneja wa mradi huo Eng. Julius Ndyamukama, ameahidi kushirikiana na wenzake katika kuhakikisha mradi huo unamalizika kwa wakati.
Kiasi cha Shilingi Bilioni 560 zinatarajiwa kutumika katika kugharamia ujenzi huo kwa awamu zote mbili.
Katika hatua nyingine Profesa Mbarawa amemsimamisha kazi Meneja wa Fedha kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA) Bw. Simba Lugando kwa kuidhinisha malipo ya ujenzi wa Uwanja wa ndege wa Songwe mkoani Mbeya kwa mkandarasi wa Kampuni ya DB Shapriea kiasi cha shilingi Bilioni 3.3 ambapo ujenzi wake haukufanyika ipasavyo.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

No comments:

Post a Comment

Pages