HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 18, 2017

WAKANDARASI WAZAWA WAIOMBA SERIKALI KUWAPA KIPAUMBELE KATIKA MIRADI YA UJENZI

Mwenyekiti wa Chama Cha Wakandarasi Tanzania, Mhandisi Lawrence Mwakyambiki akisistiza jambo kwa waandishi wahabari (hawapo pichani), jijini Dar es Salaam kuhusu Serikali kuwapa kipaumbele wakandarasi wa ndani katika miradi ya ujenzi.

Na Eliphace Marwa, Dar es salaam

Chama cha Wakandarasi Tanzania kimeiomba Serikali kuwashirikisha katika zabuni za ujenzi wa miradi mbalimbali ya umma Wakandarasi wazawa.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam  na Mwenyekiti wa Chama hicho, Mhandisi Lawrence Mwakyambiki wakati mkutano na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa mipango mbalimbali ya Serikali katika   sekta ya ujenzi hapa nchini.
Alisema kuwa wanaiomba Serikali ya Awamu ya Tano kuwashirikisha wakandarasi wa kitanzania , wakimemo wakandarasi wa madaraja yote ili waweze kujijengea kitaalamu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi ikiwemo ujenzi wa majengo mbalimbali ya Serikali mkoani Dodoma.
Mhandisi Mwakyambiki aliongeza kua hatua hiyo itasaidia kuongeza ajira kwa vijana na Kampuni za kitanzania katika shughuli za ujenzi hapa nchini.
Aidha, Chama hiyo kimeipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuwa mstari wa mbele katika kutekeleza mikakati na kusimamia sekta ya ujenzi hapa nchini.
Aidha Mwakyambiki aliongeza kuwa kutokana na uamuzi wa Serikali ya Awamu ya Tano kuhamia Dodoma ni vema wakandarasi wa ndani wakapewa fursa ya kushiriki katika kandarasi mbalimbali ambazo serikali inatarajia kuzifanya huko Dodoma.
Kwa upande Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Dar es Salaam Mhandisi John Bura alimshukuru Rais Magufuli na Serikali yake kwa kuitikia wito wa wakandarasi kwa kuwatengea miradi michache ambayo ilikwisha tangazwa.
Aliwataka wakandarasi kuunda umoja kwa ajili ya kuitekeleza kwa weledi ili kuongeza imani kwa Serikali.

No comments:

Post a Comment

Pages