HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 29, 2017

TFF YATOA NGAO MPYA YA JAMII

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetoa Ngao ya Jamii mpya kwa ajili ya kuipa Simba ambayo ilifanikiwa kuishinda Young Africans katika mchezo kuwania taji hilo uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Agosti 23, mwaka huu.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

MAJINA 8 YAPITA MCHUJO WA AWALI UONGOZI TPLB

Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imetangaza majina manane ya wagombea ambao yamepita katika mchujo wa awali kuwania nafasi mbalimbali katika Kamati ya Uongozi (Management Committee) ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini


TAIFA STARS YAANZA MAZOEZI DAR

Timu ya Mpira wa Miguu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, imeanza kujifua leo asubuhi kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Wachezaji wote kutoka klabu za Tanzania wamefika kadhalika baadhi kutoka nje ya mipaka ya Tanzania kama vile Nahodha Mbwana Samatta na Elias Maguli. Mazoezi hayo yataendelea kila siku hadi Ijumaa wiki hii.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

KAMATI YA NIDHAMU KUKETI KESHO

Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), chini ya Mwenyekiti wake Tarimba Abbas, kinatarajiwa kuketi kesho Jumatato Agosti 30, mwaka huu.
Kamati hiyo itakuwa na ajenda kadhaa ikiwamo ya mashauri yanayohusu wachezaji mbalimbali, viongozi na klabu.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

No comments:

Post a Comment

Pages