HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 08, 2017

Tigo Fiesta 2017: Tumekusomaa’ Kuiweka Elimu ya Sekondari Katika Digitali


.Tigo kuzipatia shule 50 za sekondari nchini vifaa vya elimu vya kidigitali
  • Shule tatu mkoani Arusha kuwa za kwanza kunufaika na Mradi wa Tigo wa E-shule

Dar es Salaam Sept 7,  2017- Kampuni inayoongoza ya kidigitali Tanzania, Tigo Tanzania leo imetangaza azima kubwa ya kuiweka elimu ya sekondari katika digitali, kwa kutoa vifaa vya kidigitali vya kujifunzia  kwa shule za sekondari 50 nchini kote kama sehemu ya Tigo Fiesta 2017 Tumekusomaa sherehe za kitamaduni zilizopangwa kuburudisha taifa kuanzia wikendi hii.
                                             
Kama sehemu ya jitihada zake za Tumekusoma, ambazo zinasisitizia sifa yenye nguvu kama nembo ya kampuni ya simu ambayo inaelewa vyema na kuitikia mahitaji ya wateja wake,  Tigo itakuwa inatoa vifaa vya elimu vya kidigitali kwa shule zilizoko katika mikoa 12 kati ya 15 ambako sherehe za Tigo FIesta 2017   Tumekusomaa zitakuwa zinafanyika.

Akitoa tangazo kubwa wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kujifunzia katika shule ya Sekondari Arusha jana, Afisa Mkuu wa Ufundi na Habari (CTIO) Jerome Albou, alisema kwamba azima ya kidigitali itashuhudia shule zingine 50 za sekondari ambazo mwanzo zilipatiwa computer na kuunganishwa na mtandao wa internet, pia sasa zinapokea vifaa vya elimu vya kidigitali kuongeza uwezo wa kujifunza wa wanafunzi na kuwaandaa kuwa sehemu ya kijiji cha dunia cha kidigitali. 

'Tunaishi katika ulimwengu wa kidigitali na Mradi wa Tigo wa e-shule unawawezesha wanafunzi kuwa sehemu ya ulimwengu wa kidigitali, 'alisema Albou, wakati akiwa anabainisha jitihada mpya Shule zingine mkoani Arusha ambazo zimenufaika kutokana na mradi wa e-shule ni Shule ya Sekondari ya Arusha Day na Shule ya Sekondari Ilbouru. 

Mwaka 2016, Tigo iliingia katika ubia na Wizara ya Mawasiliano, Kazi na Miundombinu kuwezesha ufunguzi wa vituo vya kuwezesha upatikanaji wa mtandao wa internet katika shule za sekondari nchini kusaidia mradi wa serikali wa e-shule kwa muda wa miaka 2.

Kama sehemu ya makubaliano, Wizara ilibainisha na kutoa orodha za shule ambazo hazina vyumba vya computer viunganishwe na pia kupewa mwongozo wa utekelezaji wa mradi. Tigo ilifadhili uendelezaji wa miundombinu katika shule nchi nzima, ikiwemo kuunganisha nyaya madarasani na ufungaji wa LAN zisizotumia waya pamoja na vituo vya kuunganisha mtandao wa internet. Hatua ya tatu ya mradi huu ni ufungaji wa sasa wa vifaa vya kujifunzia ambavyo mwanafunzi ataweza kuvipata moja kwa moja kutoka katika chumba cha computer, hivyo kufanya mtindo wao wa kujifunza kuwa wa kidigitali.

"Kupitia katika jitihada zetu za uwajibikaji kwa jamii, sasa tunatekeleza dhamira ya serikali ya kubadilisha nchi kuelekea uchumi wa misingi ya kitaluma kufikia mwaka 2025.  Kampini yetu imeazimia kuhakikisha kuwa idadi kubwa ya shule za sekondari zina huduma ya internet nchini Tanzania, pia vifaa vya  kujifunzia ili waweze kujiandaa vyema kwajili ya fursa ambazo zinakuja na mabadiliko ya kidigitali ambayo kwa sasa yanaukabili ulimwengu," Alilsema CTIO wa Tigo.

Alibainisha shule ambazo zitanufaika kutokana na mradi kuwa ni Shule ya Arusha Day, Ilbouru na Shule ya Sekondari ya Arusha katika mkoa wa Arusha; Shule za sekondari za Mwanza, Pamba na Milambo mkoani mwanza; Shule ya wasichana ya Tabora na Milambo mkoani Tabora; na Mpwapwa sekondai mkoani Dodoma.

Nyingine ni shule za sekondari Iringa na Kleruu mkoani Iringa; Shule ya sekondari Mtalewa na Shule ya sekondari ya wasichana Songea mkoani Songea; Shule ya sekondari Njombe na Mpechi mkoani Njombe; Shule ya sekondari Morogoro manispaa na Mzumbe za mkoani Morokogoro; na Shule ya sekondari Handeni na Shemsanga mkoani Tanga.

Shule zingine zitakazo nufaika na vifaa vya elimu vya kidigitali vinavyotolewa na Tigo kupitia e-shule ni, Shule ya sekondari Lyamungo na Shule ya wasichana Machame Moshi; Shule ya sekondari ya Newala na Masasi katika mkoa wa Mtwara wakati katika mkoa wa Dar es salaam shule zitakazo nufaika ni pamoja na  Mbagala, Kibamba, Benjamini Mkapa na Shule ya sekondari Makumbusho.    

'Tigo  inajivunia kuwa mbia na Wizara ya Mawasiliano, Kazi na Miundombinu na  shule kuwawezesha vijana na jamii kwa ujumla kuweza kubisha hodi katika ulimwengu wa taarifa na ufahamu, ambako watajifunza, kupanua ubunifu wao na kushirikiana na wenzao duniani kote', aliongeza Albou.

Mradi wa E-shule ni moja kati ya mikakati ya miradi ya Tigo ya kuwekeza katika jamii na mpaka sasa Tigo imesha unganisha katika mtandao wa internet sekondari 60 za umma kutoa computer 77 kwa sekondari na taasisi za elimu ya juu nchini.

No comments:

Post a Comment

Pages