HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 03, 2017

MFUKO WA PENSHENI WA LAPF YAWEKEZA KATIKA KIWANDA CHA TANGAWIZI SAME

 Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Anna Mgwhira akihutubia washiriki wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Wakurugenzi ya kiwanda cha kuchakata tangawizi kilichopo wilayani Same ambapo Mfuko wa Pensheni wa LAPF umewekeza ili kiwanda kianze uzalishaji. Hafla hiyo ilifanyika tarehe 28/09/2017.
 Meneja wa Uwekezaji na Mipango wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF Bw. Furtunatus Magambo ambaye ndio Mwenyekiti wa Bodi ya Kiwanda cha kusindika tangawizi akizungumza na wajumbe pamoja na wageni waalikwa kwenye hafla ya kuzindua Bodi iliyofanyika wilayani Same, mgeni rasmi akiwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh. Anna Mgwhira.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF Bw. James Mlowe akizungumza na waandishi wa habari baada ya uzinduzi wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kiwanda cha kusindika tangawizi kilichopo wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro, Kushoto ni Meneja wa Miradi na Miliki wa LAPF Eng. Greyson Bambanza ambaye pia ni mjumbe wa Bodi ya kiwanda hicho ambacho LAPF inawekeza kiasi cha Shs. Bilioni moja.

No comments:

Post a Comment

Pages