HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 22, 2018

Simiyu wafunika baiskeli Majimaji Selebuka Festival

NAMWANDISHI WETU, SONGEA
 
WAENDESHA Baiskeli kutoka Mkoa wa Simiyu wameng’ara katika mashindano ya Baiskeli yaliyoandaliwa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Songea Mississippi (SOMI), kupitia Tamasha la Majimaji Selebuka.
 
Mashindano hayo ya Baiskeli ya Kilomita 100 kutoka MbingaMjini hadi Uwanja wa Majimaji mjini Songea Mkoa wa Ruvuma, Masunda Duba akitumia baiskeli ya kawaida huku pia akiwa hana vifaa maalumu vya mchezo huo kama vile jezi, kofia ngumu na viatu aliwafunika wenzake ambao walikuwa na vifaa vya kisasa baada ya kushinda akitumia saa 2:53.05.
 
Duba alifuatiwa na mwenzake kutoka Simiyu, Boniphace Masunda aliyetumia saa 2:54.21 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Ipyana Mbogela kutoka Iringa aliyetumia saa 3:06.55.
 
Nafasi ya nne ilikwenda kwa Ombeni Mbilinyi pia kutoka Iringa aliyetumika saa 3:06.58 huku mshindi wa tano akiwa ni Oscar Kayombo wa Songea aliyetumia saa 3:20.53.
 
Mshindi wa sita aliibuka Aso Gadas kutoka Dar es Salaam aliyetumia saa 3:28.17, nafasi ya saba Samir Rashid pia wa Dar es Salaam saa 3:29.46, nafasi ya nane Hagai Sanga wa Mbeya saa 3:34.01 huku nafasi ya tisa ikienda kwa Elias Zawadi pia wa Mbeya saa 3:47.13.
 
Bingwa mbali ya kuzawadiwa Kombe aliondoka na kitita cha Sh. 500,000 mshindi wa pili Sh. 300,000 na wa tatu Sh. 200,000 na kutafutiwa mashindano nje ya nchi huku pia mchezaji kutoka mjini Songea, Oscar Kayombo atapata nafasi ya kutafutiwa mashindano nje ya nchi.
 
Akizungumzia siriya ushindi, Masunda alisema mchezo wa baiskeli kigezo si baiskeli bali mazoezi,
 
Tamasha la Majimaji Selebuka ambalo lilianza Julai 14 kwa shughuli mbalimbali ikiwamo maonyesho ya Wajasiriliamali, Utalii wa Ndani, Mdahalo kwa Wanafunzi, Ngoma za Asili, Riadha, Mpira wa Miguu na Riadha litafikia tamati leo kwa mechi ya kukata na shoka kati ya Simba Veterani na Yanga Veterani kwenye dimba la Majimaji ambako kiingilio ni Sh. 2,000.

No comments:

Post a Comment

Pages