HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 15, 2018

Wadau kujadili namna ya kupunguza Sumu Kuvu Tanzania

NA MWANDISHI WETU

KAMPUNI ya BASF kwa kushirikiana na Taasisi ya Kimataifa ya Kuboresha Lishe (GAIN), wameandaa warsha itakayowakutanisha pamoja wadau ili kujadiliana namna ya kupunguza kasi ya sumu kuvu nchini Tanzania.

Miongoni mwa ajenda zitakazojadiliwa katika warsha hiyo ni pamoja na Hatari kubwa ya usalama wa chakula na usalama katika nchi zinazoendelea ni sumu kuvu, ambako warsha itachunguza ufumbuzi wa kusambaa kwa kasi kwa sumu kuvu nchini Tanzania



Enock Musinguzi, ambaye Mwakilishi Mkazi wa GAIN, alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa warsha hiyo inalenga kuendeleza mkakati wa kitaifa wa kupambana na sumu kuvu, ambapo itawajumuisha pia wadau kutoka nchi nyingine.
Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), sumu kuvu ni hatari kubwa kwa usalama wa chakula na usalama katika nchi zinazoendelea.

Sumu kuvu maarufu kama Aflatoxin, ni aina ya sumu inayotengenezwa na ukungu katika nafaka iliyohifadhiwa katika sehemu ambayo kitaalamu haijakidhi vigezo vya kuhifadhia, sumu ambayo huwa na athari kwa wanadamu, wanyama na husababisha ugonjwa wa ini na saratani.

Musinguzi alibainisha ya kuwa kukosekana kwa mavuno, usafiri na utunzaji sahihi, ni miongoni mwa sababu za kuongezeka kwa kasi kwa sumu kuvu, ambako ulimwenguni, inakadiriwa kati ya watu bilioni 4 hadi 5 wapo hatarini kuathiriwa na sumu kuvu.
 


“Watoto ni miongoni mwa waathirika wakubwa, kwani sumu kuvu huwa inasababisha upunguvu wa virutubisho, udumavu na maendeleo ya ukuaji wa mtoto. Kupitia warsha hii, wadau watajifunza masuala mbalimbali kuhusiana na changamoto hii,” alisema Musinguzi.

Naye Dk. Andreas Bluethner, ambaye ni Mkurugenzi wa Chakula, Usanifu na Ubia wa BASF, alisema moja ya malengo ya warsha hiyo ni kusaka ufumbuzi wa thamani ya chakula ili kuendeleza upunguzaji wa chakula na kuongeza usalama na chakula cha lishe kufikia SDG2.

"Kama kujitolea kwetu kwa Malengo ya Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (SDG), tunaendelea kufanya kazi na wadau muhimu kwa ufumbuzi wa thamani ya chakula ili kuendeleza ufumbuzi wa kupunguza chakula na kuongeza usalama na chakula cha lishe kufikia SDG2 ya njaa ya sifuri.

“Kwa mtazamo huu, BASF na washirika wake wameunda udongo wa sumu kuvu ambao unaweza kuongezwa kwa vyakula vidogo vidogo na inaweza kupunguza upungufu wa sumu hiyo,” alisisitiza Bluethner.

No comments:

Post a Comment

Pages