HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 10, 2019

Bodi ya Ligi yajibu mapigo ratiba TPL, Simba ratiba ya moto

NA JOHN MARWA
MTENDAJI Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPBL) Boniface Wambura (pichani), amejibu mapigo kwa malalamiko ya ratiba ya Lgi hiyo akibainisha kuwa kila timu itacheza mechi 38 hivyo hakuna klabu inayopendelewa.
Wambura ameyasema hayo ikiwa ni siku moja tu mara baada ya Kocha Mkuu wa Yanga SC kutoa malalamiko ya kubanwa na ratiba ya Ligi huku watani wao SC wakiwa na viporo zaidi ya 10 wakati ambao baadhi ya klabu zimebakiza mechi nne kumaliza Ligi.
Zahera alisema wachezaji wake wanachoka sana licha ya kutumia usafiri wa Ndege kwa sababu michezo iko karibu karibu na haiwapi nafasi ya kupumzika.
Pia zahera alionyeshwa kushangazwa na michezo waliyobaki nayo wapinzani wao Simba SC kwa kuwa na michezo zaidi ya 10 ambayo hawajacheza hali inayompa ukakasi na kusisitiza kuwa ligi iko mwishoni wanapaswa Wekundu hao kucheza mechi hizo waweze kuwa sawa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Wambura alisema nikweli msimu huu wamekabiliwa na changamoto ya ratiba jambo ambalo limekuwa nje ya uwezo wao kwa uwepo wa mashindano mengi kwa baadhi ya klabu.
“Changamoto za ratiba ni kweli zipo, na tunazitambua, lakini lazima tukubali kuwa mabadiliko ya ratiba ya Ligi ya Mabingwa na Shirikisho ndo yameiasili zaidi ratiba yetu.
“Michuano hiyo ya CAF imekuwa ikifanyika kuanzia mwezi Novemba lakini sasa, CAF waliamua kubadilika na kuja kwenye mfumo wetu wa kuanza Mwezi August na kumalizika mwezi May,”amesema na kuongeza kuwa.
“Licha ya mabadiliko hayo ya CAF lakini tunmekuwa na kombe la Sport Pesa na kombe la Mapinduzi nayo yaliingia hapa kati, imekuwa ni changamoto kwetu pia ongezeko la timu kutoka 16 hadi 20 nayo imekuwa ni changamoto ukiwa ni msimu wetu wa kwanza kuwa na timu 20.
“Pia kama Taifa tulijipanga kwa timu yetu ya Taifa Taifa Stars kufuzu fainali za AFCON jambo ambalo tumefanikiwa na hili lilikula muda wa ligi kwani kuna wakati tulitumia hadi siku 21 kwa ajili ya maandalizi ya Timu hiyo.
“Pamoja na changamoto hizo limekuwa ni somo kwetu na tunaahidi kuwa msimu ujao tutakuja na ratiba ambayo haitakuwa na ukakasi kwa kila mmoja, na malalamiko yanayotolewa jamani kila timu itacheza mechi 38 hakuna itakayo cheza michezo 30,”amesema.
Lakini pia Wambura aliongeza kuwa kesho watatoa ratiba ambayo itaonyesha ni jinsi gani Simba watacheza viporo vyao na Ligi iwezealizika kwa wakati.
“Tumekaa vikao na kupitia ratiba na kesho  tutatangaza ratiba ambayo itaonyesha jinsi gani Simba na klabu nyingine zitakavyo cheza viporo vyao, ni wazi kuwa Simba watakuwa na ratiba ngumu sana na watapitia wakati mgumu lakini yote lazima tuhakikishe Ligi inamalizika mwezi May,”amesema.
Wakati wambura akitoa utetezi huo Mabingwa watetezi wameshuka dimbani mara 22 huku vinara wa ligi hiyo wakicheza mechi 30 hadi sasa.
Tayari kuna klabu zimeshacheza michezo 33 zikisaliwa na mechi tano kumaliza ligi huku Simba wakisaliwa na michezo 16 mkononi.
Simba wanakabiliwa na kibarua kizito jumamosi hii robo fainali ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika CAF CL dhidi ya TP Mazembe mjini Lubumbashi wakihitaji ushindi ama sare ya mabao kutinga nusu fainali.
Swali ni je kama Simba wanafanikiwa kutinga nusu fainali TPBL watakuja na ratiba gani kuhakikisha viporo vya Simba vinachezwa na ligi inamalizika kwa wakati.

No comments:

Post a Comment

Pages