HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 13, 2019

MAKONDA AWAPA ONYO TBA, ATAKA MIRADI YA KIGAMBONI KUKAMILIKA KWA WAKATI

NA BRIGHITER MASAKI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi mbalimbali wilaya ya Kigamboni ambapo amewaagiza Wakala wa Majengo ya serikali TBA kuhakikisha wanakamilisha Mara moja ujenzi wa majengo ya Halmashauri ya wilaya ya Kigamboni, Ofisi ya Mkuu wa wilaya na Nyumba za viongozi kabla ya Juni 30 mwaka huu.

Makonda amesema endapo wakala hao watashindwa kutekeleza agizo hilo watachukuliwa hatua ikiwemo kunyang'anywa mradi, kurudisha fedha iliyobaki na watalazimika kulipa kodi ya jengo la mtu binasi linalotumiwa kama Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

"Nimekuchukizwa na hali ya kusuasua kwa mradi huo licha ya kuongezewa muda zaidi ya mara mbili na fedha zote za ujenzi mlishapatiwa jambo linalopelekea serikali tunatumia mamilioni ya pesa kulipa kodi ya pango kwenye jengo la mtu binafsi linalotumika kama ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kigamboni, na endapo mtashindwa kutekeleza agizo hili nitachukua hatua ikiwemo kuwanyang'anya mradi,kurudisha fedha iliyobaki na mtalazimika kulipa kodi ya jengo la mtu binasi linalotumiwa kama Ofisi ya Mkuu wa Wilaya"anasema Makonda.

Akiwa katika mradi wa ujenzi wa jengo la Hospital ya Wilaya ya Kigamboni Makonda ameridhishwa na kasi ya ujenzi huo na kuagiza mkandarasi kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha jengo linakabidhiwa kabla ya Juni 30 mwaka huu.

Kwa upande wake Mratibu wa Wakala wa Majengo ya serikali Mkoa wa Dar es salaam Mhandisi Wilson Tesha amemuahidi RC Makonda kuwa wakala hao watakahikisha wanakamilisha ujenzi kabla ya Juni 30 kama walivyoagizwa.

No comments:

Post a Comment

Pages