HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 02, 2019

Wizara ya Maliasili na Utalii Kutangaza Utalii kupitia AFCON U17

 Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Prof.Adolf Mkenda (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawpo pichani) jana jijini Dodoma kuhusu namna ofisi yake imejipanga kutumia jukwaa la mashindano ya AFCON U17 kutangaza fursa za utalii zilizopo nchini katika kipindi cha mashindano hayo yatakayofanyika hivi karibuni nchini, kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi.Susan Mlawi na Kulia ni Katibu Mkuu Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw.Wilfred Kidao.  (Picha na Anitha Jonas – WHUSM).
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi.Susan Mlawi akitoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha kiasi cha Bilioni Moja  za kuendesha mashindano ya AFCON U17  yatakayofanyika hivi karibuni jijini Dar es salaam alipokuwa akizungumza na waaandishi wa habari (hawapo pichani) jana jijini Dodoma, Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Prof.Adolf Mkenda.
Katibu Mkuu Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw.Wilfred Kidao (kulia) akizungumza  na waandishi wa habari (hawapo pichani) jana jijini Dodoma kuhusu aina ya wageni wanaotarajiwa kufika katika mashindano ya AFCON U17 yatakayofanyika nchini hivi karibuni ambapo alieleza Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani Gianni Infantino anatarajia kuja katika mashindano hayo, kushoto kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Prof.Adolf Mkenda.

No comments:

Post a Comment

Pages