HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 29, 2019

Luseleko ataja sifa za kiongozi ajaye


Na Nwandishi Wetu

MCHUNGAJI wa Kanisa la GRC, Ubungo jijini Dar es Salaam Anthony Lusekelo amesema kuwa Taifa halihitaji kiongozi anayetokana na udini bali anayenadi sera.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mchungaji Lusekelo (pichani), alisema baadhi ya viongozi wa kisiasa wanaotumia nyumba za ibada kujinadi ni ishara ya kupoteza mvuto kwa wananchi.

Kiongozi huyo wa Kiroho alisema, Taifa linahitaji kupata mgombea ambaye ananadi sera zake ambazo zitakubalika na wananchi na sio kutumia nyumba za ibada kutafuta kura.

“Hili Taifa halina dini na wala halihitaji mgombea anayetokana na dini fulani bali aliye na sera zinazokubalika ukiona mgombea anatumia nyumba za ibada kutafuta kura huyo hana nguvu za kisiasa,” alisema.

HAMAHAMA

Mchungaji Lusekelo alionyesha kuchukizwa na baadhi ya viongozi wanaohama hama vyama vya siasa na kusema kuwa hatua hiyo inapoteza uaminifu kwa wananchi waliowachagua.

Hivi karibuni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani wamekuwa wakihama vyama hivyo na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) hatua inayosababisha kurudi katika uchaguzi mdogo.

, siasa sio uadui lakini kitendo cha baadhi ya viongozi kushindwa kusimamia kauli zao na kuamua kujiondoa katika vyama vyao vinapoteza uaminifu.

Aliwataka viongozi hao kuhakikisha wanatumia vyama vyao na kuyasimamia yale wanayoyaahidi kwa wananchi kwa kuhimiza umoja, mshikamano na uzalendo.

“Kuhamahama sio shida lakini kwangu mimi nachukizwa na vitendo hivyo kwani inaonyesha wazi viongozi hao hawawezi kuyasimamia yale wanayoyaahidi,” alisema.

UCHAGUZI

Mchungaji Lusekelo alisema, kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa hauna tija ni kutaka kuihamsha na kulisumbua Taifa.

Alisema kuwa kuna sherehe nyingi Rais John Magufuli ameweza kuzifuta hivyo kama angeweza kumshauri kiongozi huyo uchaguzi huo ungesogezwa na kufanyika mwakani 2020 ili kupunguza gharama.

“Kama ningekuwa Waziri Mkuu au Waziri wa Tamisemi ningeshauri na kumuomba Rais awaache viongozi waliopo madarakani wa serikali za mitaa wakaendelea wao na uchaguzi tukaufanya mwaka 2020,” alisema.

Kiongozi huyo wa kiroho alisema, hatua hiyo itaweza kulifanya Taifa likaendelea kupumua na viongozi wakaendelea kusaidia kufikia maendeleo ya uhakika.

Kumkosoa Rais

Alisema kuwa sio maadili kumkosoa kiongozi wa nchi kihuni na kuwataka wale wanaokosoa kusubiri kiongozi huyo atakapoondoka madarakani watumie fursa hiyo kumkosoa.

Aliwataka wanaohitaji kukosoa kuwaachia wabunge ambao wanaweza kutumia muhimili huo kukosoa kwa weledi.

No comments:

Post a Comment

Pages