HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 08, 2019

JESHI LA POLISI DSM, DCI WAANZA KUCHUNGUZA VIDEO INAYODHANIWA YA ASKOFU GWAJIMA

JESHI la Polisi Kanda Maluum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), limeanza uchunguzi wa picha na video ya ngono inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii, inayodhaniwa kuwa ya Askofu Josephat Gwajima.
Kamanda Lazaro Mambosasa.
Jana Mei 7, kulianza kusambaa kwa video hiyo, kutoka kwa watu wasiojulikana kwenye mitandao ya kijamii, zikidhaniwa kuwa ni za Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, akiwa anafanya ngono na mwanamke asiyefahamika.

Kwa mujibu wa taarifa za Jeshi la Polisi zilizotolewa mchana mchana huu, jeshi hilo linakiri wazi kuwa Askofu Josephat Gwajima sio mtuhumiwa wa picha hizo, bali ni muathirika na kwamba jambo hilo linaweza kufanywa na mtu yeyote kwa lengo la kumchafua kwa waumini wake.

“Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limeanza uchunguzi wa picha na video za ngono mara moja na linapenda kuwaarifu wananchi kuwa, Gwajima sio mtuhumiwa, bali muathirika wa tukio hilo, kwani ni jambo linaloweza kufanywa n amt yeyote ili kumchafulia kwa waumini wake,” ilisema taarifa hiyo.

Jeshi hilo likaenda mbali katika taarifa yake hiyo iliyosainiwa na Kamanda Lazaro Mambosasa, kwa kuonya kuwa wananchi waache tabia ya kusambaza video na picha zinazokinzana na maadili, huku likiwataka waumini wa Askofu Gwajima kuwa watulivu wakati uchunguzi wa kumbaini aliyefanya ukiendelea.

Baada ya kusambaa kwa video hizo jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, alitoa taarifa za jeshi lake kumtaka Gwajima aripoti Makao Makuu ya Polisi, agizo alilopaswa kulitekeleza leo asubuhi, vinginevyo angesakwa na kukamatwa popote.

“Tayari Askofu Josephat Gwajima ameitwa Polisi kwa ajili ya kuhojiwa na ataripoti kesho asubuhi (yaani leo), akichelewa ataamatwa na tumemuita sababu hakuna aliyelalamika, lakini tumeona ni kitendo cha ukiukwaji wa maadili, awe Askofu ama mtu wa kwaida, ule ni unyama,” alisema Kamanda Mambosasa.

Akizungumzia tukio hilo leo, kwa waandishi wa habari, mbele ya maaskofu, wachungaji wa makanisa mbalimbali, na waumini wake kanisani kwake Ubungo jijini Dar es Salaam, Askofu Josephat Gwajima amezihusisha video hizo na kampeni chafu za kumnyamazisha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, utakaofanyika nchini mwakani.
Mchungaji Gwajima.

Gwajima akaenda mbali kwa kulishangaa Jeshi la Polisi Kanda Maalum kumuita Polisi, badala ya kuanza uchunguzi wa kumbaini aliyefanya kazi ya ‘kuedit’ picha na kuchanganya matukio kisha kumuhusiha yeye kwa lengo la kumchafua.

“Nimeitwa Polisi, yaaani niliyejurihiwa ajalini alafu niende Polisi, badala ya walionijeruhi? Wamtafute huyu mtu wampate. Haiwezekani nichafuliwe mimi, waliofanya hivyo wasikamatwe, ila akichafuliwa mtu fulani akichafuliwa muhusika anapatikana haraka,” alisema huku akishangiliwa na waumini wake.

No comments:

Post a Comment

Pages