HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 08, 2019

ASKOFU GWAJIMA: SIO MIMI, NI WANASIASA WANAJARIBU KUNICHAFUA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2020

 Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Gwajima, akizungumambele ya maaskofu, wachungaji wa makanisa mbalimbali, na waumini wake kanisani kwake Ubungo jijini Dar es Salaam leo, kuhusu video za udhalilishaji zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Gwajima, akizungumambele ya maaskofu, wachungaji wa makanisa mbalimbali, na waumini wake kanisani kwake Ubungo jijini Dar es Salaam kuhusu video za udhalilishaji zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii.
  Mke wa mchungaji Gwajima akizungumzia tukio hilo.


NA MWANDISHI WETU, DAR
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Gwajima, amejitokeza hadharani leo kuzikana video za udhalilishaji zilizosambaa mitandaoni, akizitaja kama zao la picha za kutengeneza na watu maalum ili kumchafua na kujaribu kumnyamazisha.

Akizungumza na waandishi wa habari, mbele ya maaskofu, wachungaji wa makanisa mbalimbali, na waumini wake kanisani kwake Ubungo jijini Dar es Salaam, Gwajima amezihusisha video hizo na kampeni chafu za kumnyamazisha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, utakaofanyika nchini mwakani.

“Kumekuwa na mbinu chafu za watu, wanaofikiria tufanye hiki ili kumnyamazisha Gwajima, sasa nawaambia hamuwezi kuninyamazisha. Ni mwanaume gani anaweza kufjamiiana na mke ama mpenzi wake, huku akijirekodi mwenyewe, akatuma mwenyewe mitandaoni,”? amehoji Gwajima.

Amebainisha ya kwamba: “Ukiangalia video hizo, utagundua kwa mwili wa anayeshiriki vitendo hivyo ni mwingine, kichwa cha mwingine, na hata mkono ni wa baunsa, tofauti na wangu. Zilizotumika ni picha mgando kuunganisha na picha zingine ili kufanikisha walichopanga.”

“Napunguzwa nguvu kisa Uchaguzi Mkuu wa mwakani, wakijua kuwa wakati wa mchakato huo nitawatesa, sasa hapa hapunguzwi mtu nguvu, waliofanya hivyo walichoithibitishia jamii tu ni kuwa mimi ni mwanaume kamili, hawajanichafua. Hakuna mwanaume kamili asiyeshiriki tendo hilo, ila hufanywa faragha,” akasema.

Aidha, Gwajima amelishangaa Jeshi la Polisi kwa kitendo cha kumuita kuhojiwa, na kwamba walichopaswa kufanya ni kuwasaka wachafuzi na kuwawajibisha kwa mujibu wa Sheria za Makosa ya Mtandao na sio kumuita yeye aliyejeruhiwa.

“Nimeitwa Polisi, yaaani niliyejurihiwa ajalini alafu niende Polisi, badala ya walionijeruhi? Wamtafute huyu mtu anayemiliki akaunti ya Instagram kwa jina la Original, wampate. Haiwezekani nichafuliwe mimi, waliofanya hivyo wasikamatwe, ila akichafuliwa mtu fulani akichafuliwa muhusika anapatikana haraka.

“Nitasimama imara na nitakuwa zaidi ya nilivyokuwa, nitasema zaidi ya uchaguzi uliopita. Nitapambana na sitokufa, sifi, sitotekwa na sitoweza kuteswa na yetote,” akasma Gwajima, ambaye aliambatana na mkewe, ambaye pia alizungumza na kusema anamjua na kumuamini mumewe na haamini katika anayozushiwa.

Baada ya kusambaa kwa video hizo jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, alitoa taarifa za jeshi lake kumtaka Gwajima aripoti Makao Makuu ya Polisi, agizo alilopaswa kulitekeleza leo asubuhi, vinginevyo angesakwa na kukamatwa popote.

“Tayari Askofu Gwajima ameitwa Polisi kwa ajili ya kuhojiwa na ataripoti kesho asubuhi (yaani leo), akichelewa ataamatwa na tumemuita sababu hakuna aliyelalamika, lakini tumeona ni kitendo cha ukiukwaji wa maadili, awe Askofu ama mtu wa kwaida, ule ni unyama,” alisema Kamanda Mambosasa.

No comments:

Post a Comment

Pages