HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 02, 2019

BONDIA ANTHONY JOSHUA ACHAKAZWA, AVULIWA MIKANDA YA WBA, WBO NA IBF

 Bondia Muingereza Anthony Joshua, akiwa ameangukia kamba baada ya konde zito kutoka kwa mpinzani wake Andy Ruiz Jr wa Mexico, wakati wa pambano masumbwi usiku wa kuamkia leo. (Picha na Daily Mail).
 Bondia Ruiz Jr akiwa na wapambe wake na mikanda aliyotwaa wakishangilia ushindi dhidi ya Joshua.
 Joshua chali aisee.
 Mwamuzi akimuangalia Joshua baada ya kutupwa sakafuni raundi ya tatu.
 Mwamuzi akimuangalia Joshua baada ya kutupwa sakafuni raundi ya tatu.
 Ruiz Jr akirushiana makonde na Joshua wakati wa pambano lao.
Ruiz Jr akitupiana makonde na Joshua wakati wa pambano lao.
 Ruiz Jr akiwa amekalishwa na Joshua kunako raundi ya tatu.


NEW YORK, MAREKANI

BONDIA machachari wa kimataifa wa England, Anthony Joshua, amepoteza mikanda yake ya ubingwa wa Dunia, baada ya kukubali kipigo cha raundi ya saba kutoka kwa Mmexico Andy Ruiz Jr, kwenye Ukumbi wa Madison Square Garden, New York.

Pambano hilo la uzaji wa juu, limeunguruma usiku wa Jumamosi kuamkia Jumapili jijini New York, Marekani, ambako kipigo kimemfanya Joshua maarufu kwa la AJ (ambalo ni kifupisho cha majina yake), kupoteza mikanda mitatu ya Dunia ya WBA, WBO na IBF.

Anthony Joshua alilianza pambano hilo taratibu na kuibua hofu ya kutimia kwa tambo zake za kutopoteza pambano hilo alizokuwa akizitoa kuelekea mtifuano huo na mwanzo wake huo haukushangaza kumuona akilambishwa sakafu kunako raundi ya tatu, ingawa alimudu kuendelea naye kumkalisha Ruiz Jr.

Kwa ushindi huo, Ruiz Jr – ‘bonge mwenye mwili nyumba na minyama uzembe ya kumwaga,’ ameweka rekodi ya kwa bondia wa kwanza wa Mexico kuwa bingwa wa Dunia wa masumbwi ya uzani wa juu. Mwamuzi wa pambano la jana usiku, alikuwa ni Mike Griffin.
Daily Mail

No comments:

Post a Comment

Pages